HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Sunday 19 June 2016

List ya nchi 11 zinazoongoza kwa amani na usalama duniani



List ya nchi zenye usalama zaidi duniani kwa mwaka 2016 imetoka hivi karibuni ambapo nchi 11 zimetajwa kuongoza kwa kuwa na usalama na amani zaidi. List hiyo ilihusisha mataifa 163 ambapo ilijulikana yale yanayoongoza kwa amani na usalama pamoja na yale ambayo ni hatari zaidi kuishi kutokana na hali ya usalama.
Toleo la 10 la kila mwaka lililotolewa June 8 2016 limetaja viwango vya amani na usalama kupitia system ya ramani  shirikishi ya mtindo wa rangi za kujificha, kila nchi ilitolewa alama kati ya 5, nchi zenye alama chini ya 5 ndio zenye hali kubwa ya usalama na amani na zilizoizidi namba 5 ndizo hatari zaidi.
Ulifanyika uchambuzi wa mambo 23 chini ya makundi matatu, Usalama na amani ya taifa, Migogogro ya ndani na nje ya nchi pamoja na huduma za kijeshi. Nchi ya Iceland inatajwa kuongoza kwa kuwa na amani zaidi kutokana na utulivu wa jamii yake.
Nchi za ulaya zinaongoza kutokana na kutokuwa na migogoro ya ndani na nje pamoja ya hali ya utulivu kwa ujumla, japokuwa Afrika inasifika kuwa na nchi zenye  amani hakuna hata nchi moja ya Afrika iliyopo katika list. Hata hivyo imetoka pia list ya nchi ambazo usalama wake ni wa chini sana ambapo nchi za Syria, Iraq, Sudan Kusini, na Afghanistan .
ORODHA YA NCHI 11 ZINAZOONGOZA KWA KUWA NA USALAMA NA AMANI ZAIDI DUNIANI
11.Finland – 1.429
10. Slovenia – 1.408
9. Japan – 1.395
8. Canada – 1.388
7. Switzerland – 1.37
6. Czech Republic – 1.36
5. Portugal – 1.356
4. New Zealand – 1.287
3. Austria – 1.278
2. Denmark – 1.246
1. Iceland – 1.192


No comments:

Post a Comment