BILA
shaka mpenzi msomaji umzima buheri wa afya na muda huu unanifuatilia
katika busati letu zuri la mahaba, mahali tunapojuzana na kuelimishana
mambo kadha wa kadha yahusuyo mapenzi na uhusiano. Nakukaribisha kwa
moyo mkunjufu tuijadili mada yetu ya leo kama inavyojieleza hapo juu.
Ni
ukweli usiopingika kuwa katika zama hizi za sayansi na teknolojia,
maumivu ya mapenzi yameongezeka maradufu. Kile tunachoamini kuwa ni
maendeleo, kinazidi kuzitesa hisia na nafsi zetu na suala la kutendwa,
kuumizwa, kuvunjika mioyo au kusalitiwa, linaonekana kuwa fasheni siku
hizi.
Kinachowasumbua wengi ni kushindwa kuelewa nini cha kufanya
baada ya kuangukia katika dimbwi la maumivu ya kimapenzi. Hebu kila mtu
ajiulize:
Umewahi kukuta SMS ya mapenzi kwenye simu ya mpenzi wako
akimtumia mtu mwingine tofauti na wewe? Ulijisikiaje uliposikia mtu
mwingine akiitwa majina mazuri ya kimapenzi na mpenzi wako, pengine
kuliko hata yale ambayo huyatumia kwako? Ulichukua uamuzi gani?
Kila
mtu ataeleza anavyojua yeye lakini ukweli ni kwamba wengi hawajui
kukabiliana na maumivu hata yale yanayosababishwa na maisha ya kawaida.
Kwa kuwa maumivu, usaliti, kuvunjika kwa mioyo na uongo katika mapenzi
ni jambo ambalo kwa kiasi kikubwa halikwepeki katika zama hizi, jambo la
msingi ni kujua nini cha kufanya baada ya kutokewa na dhoruba hizo za
kimapenzi.
Hebu msikilize msomaji wangu, Jane wa Ilala Bungoni jijini Dar, alivyokuwa analalama:
“Wiki
nzima inaisha sasa, siendi kazini, chakula hakipandi, usingizi sipati
wala sitamani kitu chochote, kitu pekee ninachokifanya ni kulia usiku na
mchana, naomboleza na kulalama katika kila sekunde inayopotea mpaka
natamani kujiua, sioni tena thamani ya kuishi, nayachukia mapenzi,
nawachukia wanaume,” alisema Jane huku akilia kutokana na kutendwa na
mwandani wake aliyemsaliti kwa kutoka na rafiki yake kipenzi.
Yawezekana
Jane hayuko peke yake, wapo wengi ambao wanateswa sana na mapenzi
lakini hawana sehemu ya kuyatoa maumivu yao, wanaumia ndani kwa ndani,
miili yao inadhoofika kila siku, hawana furaha japokuwa wanapata
mahitaji yote muhimu, chanzo kikuu kikiwa ni mapenzi.
Hapo ndipo ninapoona umuhimu wa kila mmoja kujua namna ya kusimama tena pale anapoangushwa na maumivu ya kimapenzi.
Zifuatazo ni mbinu ambazo zitakusaidia kuyabadilisha maumivu yako ya kimapenzi kuwa furaha.
JIFUNZE KUSAMEHE NA KUSAHAU
Hakuna jambo ambalo hutuliza fikra
na hisia za mapenzi kama kukubali kumsamehe yule aliyekuudhi kabla hata
hajakuomba msamaha na kuamua kusahau yote yaliyotokea. Yawezekana wengi
mtasema haiwezekani. Inawezekana na wote waliojaribu mbinu hii
walifanikiwa.
Marafiki, lazima kila mmoja aelewe kwamba
unapokasirika au kuumizwa, anayeteseka siyo yule aliyekusababishia
maumivu bali ni wewe mwenyewe. Hasira au maumivu ya kimapenzi huwa kama
moto mkali ambao huitafuna taratibu nafsi ya mhusika.
Ukisamehe
maana yake unaupa moyo na akili yako nafasi ya kupata sehemu ya kutulia
na kuuzima moto ambao tayari ulishaanza kukolea ndani yako.
FAHAMU MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHA UPENDO UKAPUNGUA KWA MPENZI WAKO

1. UGOMVI WA KILA SIKU
Kwenye Ulimwengu Wa Mapenzi Hakuna Kitu Kibaya
Kama Kutoweka Kwa Amani Kaa Ukijua Mapenzi Ni Matamu Na Yanaraha
Iliyoambatana Na Furaha Hakuna Mtu Anaependa Kuishi Bila Ya Kuwa Na
Furaha Hivyo Ikitokea Katika Mahusiano Wapenzi Hawapatani Na Kila Mmoja
Wao Hataki Kukubali Kosa Wote Wanajiona Wapo Sahihi Halafu Mwisho Wa
Siku Wanapatana Ghafla Bila Kuombana Msamaha Ni Wazi Kabisa Kosa Bado
Litakuwa Halijarekebishwa Hivyo Ni Rahisi Kutokea Tena Ugomvi Na
Ikitokea Kila Siku Penzi Lenu Linatawaliwa Na Ugomvi Nirahisi Penzi
Kukosa Muelekeo Na Kila Mmoja Wenu Akahisi Hapati Amani Ya Pumziko La
Moyo Kwa Mpenzi Wake Hivyo Mnaweza Kujikuta Upendo Unapungua Katika
Penzi Lenu Na Matokeo Yake Moyo Wako Utakuwa Bado Haujapata Kimvuli Cha
Burudani Za Mahaba Utajiwa Na Fikra Za Kutaka Kumtafuta Mpenzi Mwingine.
2. KUTOKUBALI HALI HALISI YA MPENZI WAKO:
Hii Ni Moja Kati Ya Sababu Kubwa Inayopunguza
Mapenzi Kwa Kiasi Kikubwa, Walio Wengi Katika Mahusiano Siku Zote
Hutegemea Faida Tu Kwa Upande Wake Pasipo Kumjali Mwenzake Zaidi Hili
Hutawala Katika Upande Wa Kifedha, Unaweza Kumkuta Mtu Anampenda Mpenzi
Wake Pindi Awapo Na Hela Na Kama Ikitokea Siku Mpenzi Wake Kakosa Hela
Basi Inaweza Kutokea Hali Ambayo Si Yakawaida. Kikubwa Naomba Utambue
Kuwa Mapenzi Sio Pesa Ila Pesa Ni Sehemu Moja Wapo Ya Mapenzi Ambayo
Hutumika Katika Njia Ya Kuboresha Mapenzi Nachoweza Kukwambia Jaribu
Kuwa Muelewa, Kubaliana Na Hali Halisi Ikitokea Unashida Ya Pesa Au Kitu
Chochote Toka Kwa Mpenzi Wako Muombe Kama Anacho Atakupa Au Kukununulia
Na Kama Hana Atakuambia Kwamfano: "Mpenzi Kwa Sasa Hali Yangu Iko Chini
Kidogo Naomba Univumilie Kati Ya Hizi Siku 2 Nitakupa" Utakapo Ambiwa
Hivi Kuwa Nasubira Mvumilie Ila Kama Hutojali Hali Ile Na Ukaenda
Kinyume Na Maombi Yake Niwazi Kabisa Hisia Zake Zitamtuma Wewe Si Mkweli
Kwake Na Nirahisi Kupunguza Upendo Kwako
3. KWENDA KINYUME NA HISIA / MATAKWA YA MPENZI WAKO:
Mpendwa Napenda Ufahamu Katika Mapenzi Kila
Mmoja Huwa Na Tabia Yake Na Sheria Zake Katika Mapenzi Hivyo Ni Vizuri
Mkiwa Kama Wapenzi Katika Mahusiano Yenu Muweze Kusomana Tabia Na Kila
Mmoja Wenu Aweze Kutambua Mpenzi Wake Anapenda Nini Na Nini Hapendi
Tukija Katika Upande Wa Sheria Pia Ni Vizuri Kama Kila Mmoja Wenu Aweze
Kumueleza Mwinzie Vitu Anavyotaka Vifuatwe Katika Mahusiano. Mapenzi
Yanaweza Kupungua Katika Hili Iwapo Kama Itatokea Kuna Mmoja Wapo Kati
Yenu Anahitaji Afanyiwe Vitu Fulani Lakini Vinakuwa Havitekelezwi Kwa
Mfano: Mpenzi Wako Anaweza Akakuomba Kushiriki Tendo La Ndoa Akiwa Na
Hamu Anakwambia "Dear Leo Naham Nawewe Mpenzi Nahitaji Kulifurahia Penzi
Lako Usiku Wa Leo" Unamjibu "Umeisha Anza Nawewe Mimi Sijisikii
Bwana!". Kinapotokea Kitu Kama Hiki Ni Dhahiri Kwamba Umeshindwa
Kumtimizia Mpenzi Wako Mahitaji Yake Ndipo Upendo Wake Kwako Utaanza
Kupungua Hatima Yake Ataamua Kutafuta Mtu Mwingine Kwani Atahisi Kama
Kwako Hapati Anavyovitaka.
Je unasumbuliwa na tatizo la kutodumu na mpenzi mmoja?
Ni
matumaini yangu marafiki mtakuwa mko poa na mnaendelea na majukumu ya
kazi za kila siku. Kama kawaida kupitia safu hii tunapata kujifunza
yahusuyo mapenzi.
Ninapoandika
makala haya, najaribu kujenga picha kwa vijana wangu wakali kunako
anga la muziki wa Bongo Fleva, Ali Kiba na Judith Wambura ‘Jide’
walipoimba; hakunaga mapenzi yale… kupendana ni zama za kale!... siku
hizi kwa kudanganyana, mvulana msichana, ishakuwa poapoa tu.
Kizazi
cha zamani hakikupata shida sana katika hili. Kilisubiri muda muafaka
ufike ndipo mtu athubutu kufanya maamuzi ya kuingia katika uhusiano
ambapo ndani ya muda mfupi basi ndoa ilichukuwa nafasi.
Kizazi
cha sasa hivi, kimetawaliwa na tamaa, vijana wanaingia katika uhusiano
wakipelekwa na tamaa za kimwili pasipo kutazama umri na madhara ya
kukurupukia mapenzi. Matokeo yake sasa, ndiyo pale unapoona vijana
wanateseka katika kumpata mke au mume wa maisha.
Ukweli
ni kwamba, tatizo na kutodumu na mpenzi mmoja kwa sasa ni sugu haswa
kutokana na mapenzi kuzidiwa nguvu na fedha au hulka ya mmoja wenu.
Ilivyo
sasa, ni rahisi sana mtu kuachana na mpenzi huyu kuhamia kwa yule
akitegemea kupata kitu fulani ambacho amekuwa akikikosa kutoka kwa
mpenzi wake.
Ni
vema sasa, tukajiuliza nini faida ya huko kuhamahama kwa kila kukicha?
Matokeo yake ni nini? Hapo ndipo utagundua kwamba yule unayemfuata
ukidhani atakupa suluhu ya tatizo ulilokuwa nalo kwa mpenzi wako wa
awali tayari na yeye ameshatendwa sana, moyo wake hauwezi kuwa kwako
moja kwa moja.
Cha
msingi hapa ni kufahamu alama za nyakati na kuweza kupambanua mambo
ili kuendana na mazingira uliyonayo. Vipengele vifuatavyo vitakusaidia
kutambua nini cha kufanya katika ulimwengu huu ambao mapenzi yanaanza
kupoteza thamani yake ili kuweza kufikia malengo.
1. TAZAMANENI VIGEZO
Kumtazama mpenzi wako inamaana kubwa sana katika uhusiano, haswa kwenye
hatua za mwanzoni kabla hujafanya maamuzi kuwa mke au mume. Inakupasa
rafiki kutazama aina ya mwanaume au mwanamke utakayemtaka atakuwa
sahihi kudumu katika uhusiano kwa muda gani?
Jiwekee
malengo ya karibu kwa kutazama utayari wa mwenzako. Tumia akili yako
ya kuzaliwa kuweza kupambanua mambo ambayo hayahitaji elimu ya chuo
kikuu.
Kabla
ya kuanzisha uhusiano mpya tayari utakawa umeshaona mengi siku
zilizopita kitu ambacho kitakusaidia kumpima mwenzi wako kama yupo
tayari kuanzisha safari mpya ya mapenzi yenye malengo.
2. USIHARAKIE PENZI
Marafiki wengi kwa sasa wanapoingia katika uhusiano huwa wanafuata
tendo la ndoa tu. Ni bora ukasubiri kwa muda fulani ili uweze kumfahamu
mwenziyo anamsimamo gani kabla hujazama ndani ya penzi.
Tendo la ndoa ni kitu cha mwisho katika mapenzi. Kabla hujafikia
kufanya tendo hilo ni vema ukawa tayari umeshapita hatua kadhaa
zitakazoweza kukusaidia mwenendo wa tabia za mwenzi wako kabla safari
yenu haijaota mizizi.
3. MUWEKE KARIBU
Ukaribu katika uhusiano unasaidia sana, hapo itakusaidia kutambua vitu
gani mwenzio anafurahi kuvipata kutoka kwako na vipi havipendi.
Yawezekana kabisa ukampatia au kumfanyia kitu anachotaka ili iweze
kukusaidia mbinu nyingine za kumfanya awe karibu na wewe utamfahamu
zaidi.
Ukaribu
huo, utasaidia kumfahamu mpenzi wako kwa vitendo, utampima kama moyo
wake ni wa kuridhika ama la! Huwezi kumfahamu mtu wakati muda mwingi
unakuwa bize na mambo yako, tenga muda kila wakati uweze kuwa na mpenzi
wako ili uweze kupata mambo mengi kutoka kwake.
4. JIFUNZE TABIA ZAKE
Unapojifunza tabia za mpenzi wako, ni rahisi udhaifu alionao katika
uhusiano. Yawezekana ukabaini kitu ambacho ni rahisi kuweza
kumbadilisha tabia zake pasipo hata yeye kujua kama unambadilisha.
Tabia ya mtu huwa haijifichi hata siku moja, hata kama ataamua kuficha
makucha lakini mwisho utakuja gundua. Wengi wanaingia katika mapenzi
kwa ajili ya kupata masilahi fulani huwa hawapendi kucheleweshewa hivyo
atajitoa mwenyewe kabla hata moyo wako haujazama katika penzi lake.
5. ZUNGUMZENI UKWELI
Ukweli huwa ndiyo silaha kubwa katika mapenzi. Mmoja wenu akiwa muongo
hakika penzi haliwezi kufika mbali. Jaribu kumwambia mpenzi wako ukweli
wa hali uliyonayo huku ukitazama mapokezi yake.
Kwa
mtu mwenye mapenzi ya dhati siku zote huamini katika ukweli. Epuka
kuongopa, jadilini mambo yenu. Wekeni mikakati ya penzi lenu ili muweze
kufikia malengo.
Ni
vema ‘ukamchana live’ mpenzi wako kwa kumwambia, “najua unajua kama
najua sasa kwa nini tudanganyane?” Wakati huo kila mtu ataona ipo haja
ya kutulia sababu kama ni ujanja basi wote mmeshapitia nyanja zote
hivyo mnapoamua kutulia basi mnatulia kweli.
USISTADUU, UBRAZAMENI NA MAPENZI YA KICHINA

MAPENZI yamekuwa magumu. Ni mzigo mzito kuubeba. Yanaendelea
kujeruhi wengi, bado ni mateso kwa wengine. Sasa hivi, asilimia kubwa ya
watu, inaamini kwamba kupata mwenzi sahihi wa maisha ni ndoto za
alinacha. Ni kamari, ni bahati nasibu.
Maendeleo yamekuja na
mambo leo. Kile kinachoonekana ni Uzungu, kimeathiri kwa kiasi kikubwa
ustaarabu wetu. Mila na desturi zetu, vimepokwa na utandawazi uliotujia.
Hii inamaanisha kwamba uhusiano wa kimapenzi wa sasa, hauendani na sura
ya utamaduni wetu.
Vijijini kuna unafuu japo na kwenyewe fujo
zimeshaingia na mambo yameshabadilika. Mijini ndiyo matatizo yenyewe.
Ulimwengu wa digitali na fursa za mitandao zinatutia wazimu. Tunataka
kuiga mitindo ya maisha ya wenzetu, matokeo yake tunageuka watumwa wa
mapenzi.
Hayakuletwa mapenzi ili yawaumize watu, yapo kwa ajili ya
kutoa faraja ndani ya jamii. Yalivyo ni kwamba baada ya misukosuko ya
kimaisha, vurugu mechi za kusaka riziki na mihangaiko mingine ya
kimaisha, angalau unaweza kusahau yote unaporejea kwa mwenzi wako.
Hata
hivyo, mapenzi hugeuka matatizo pale ambapo kazini umeondoka pakiwa
moto, unarudi nyumbani nako pia unakuta moto. Unakosa sehemu ya kwenda
kujishikiza. Faraja inaota mbawa. Hapa ndipo tafsiri ya mapenzi
inapokosa mashiko. Jitazame, muangalie na mwenzako!
Japo ni ukweli
usiopingika kuwa mapenzi siku zote hayapo tambarare hata kwa wenza
waliostaarabika, ila katika kundi la mabrazameni na masistaduu ni
mtihani. Kuna usemi kwamba glasi hugongana kabatini, nakubaliana nao
lakini kwa makundi hayo ni pasua kichwa.
Mabrazameni na masistaduu ni
zao la mapenzi ya Kichina, yaani uhusiano bandia. Inawezekana akiwa
kwako akajilegeza kama amefika, kumbe anao wengine wengi. Hili ni janga
zito kwa maisha ya sasa. Uaminifu haupo, uzinzi na usaliti vimekuwa
fasheni ya kutukuzwa.
Wengine siyo masistaduu wala mabrazameni, wapo
kawaida au pengine wana muonekano wa heshima mno. Hata hivyo, ukichimbua
hulka zao ndiyo utachoka. Ni wakali wa kuwapanga foleni, akitoka kwa
huyu anakwenda kwa yule. Mapenzi yametawaliwa na rangi ya Shetani.
Wapo
wanaobadili wapenzi kwa sababu za tamaa, lipo kundi linaloamini miili
yao ni mtaji wa kupata fedha, wengine shida za maisha zikasababisha
uamuzi huo wa kujidhalilisha, wapo ambao ni tabia. Bila kugusa huku na
huko hatosheki. Makundi yote hayo yamezingirwa na Ibilisi.
Mume wa
mtu, anapewa sifa ya ‘uchapaji’ wa vidosho. Kwamba anajua kuwapanga kila
kona. Nyumba za kulala wageni, anaingia kama nyumbani kwake. Yaani
wanamjua, ni mteja wao hodari. Akifika, wanampeleka kwenye chumba
anachokipenda.
Wapo wanaopiga simu, yaani namba za nyumba za kulala
wageni zimejaa kwenye simu yake. Akijibiwa kwamba Sinza Kumekucha hakuna
vyumba, anapiga Vatican, nako akikosa anajaribu Mori. Inahitaji sala na
dua kuishi na mtu wa aina hiyo. Kuna mawili, kama hatakupa maradhi,
omba usijue tabia yake, atakuua kwa presha.
Mke wa mtu mkali wa
mafiga matatu mpaka matano. Anaita vidumu. Anaingia hoteli na gesti bila
woga. Wapo wanaodiriki kuwaingiza wanaume ndani ya nyumba zao, wakati
waume zao wakiwa hawapo. Balaa likamkuta yule mwanamke wa Kenya,
akagandiana na mwanaume aliyemuingiza chumbani kwake, juu ya kitanda
anacholala na mumewe.
Wengine ni ujasiri wa asili, wapo wanaofanya
hivyo kwa sababu wanaona fasheni. Katika kundi hili wanaorukaruka,
wakijiona ni fasheni ndiyo shabaha yangu kubwa. Itapendeza zaidi mapenzi
yakikaa kwenye mstari wake ulionyooka. Maana halisi isipindishwe.
Kama ambavyo Jennifer Lopez anabadili wanaume Marekani,
Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili

Kuna somo kubwa mno kwenye
mada hii kwa sababu wengi wapo kwenye mateso makubwa ya kimapenzi
kutokana na makosa yao wenyewe.
Ukisoma ujasiriamali, utaelekezwa kwamba mafanikio yako yatatokana
pia na namna ulivyo na nidhamu katika fursa unazopata. Inawezekana ukawa
na bahati kwenye maisha lakini utabaki kuwa si lolote endapo hutatumia
nafasi zako vizuri.
Kama maisha, ndivyo yalivyo mapenzi. Hayatanyooka, wala hayatakaa
vema upande wako ikiwa hutakuwa na heshima kwa fursa utakazopata. Si
suala la ujana au kujipanga, muhimu kwako ni kuheshimu kile kilichopo
jirani yako. Zingatia: Mapenzi ni changamoto nzito.
Ukichezea penzi lako leo kwa sababu unazozijua wewe, tambua kwamba
halitakaa kwako daima. Kama yalivyo maisha kwamba yapo mfano wa kioo,
ukiyachekea yanacheka, ukiyanunia nayo yananuna. Ndivyo na mapenzi
yalivyo. Ukiyachezea, nayo yatakuchezea kweli.
Unapaswa kuyaheshimu. Heshima ya mapenzi ni kumtunuku mapenzi ya
kweli huyo ambaye amekujia na mapenzi yake. Umethibitisha anakupenda
kweli, sasa kinachokuwasha nini mpaka uunyanyase moyo wake? Fumba macho,
mara nyingi bahati huwa haiji mara mbili.
Inawezekana mwenzi wako wa leo ndiye mwenye mapenzi ya kweli. Ila
wewe unausimanga moyo wake kwa sababu hana fedha. Unakwenda kuabudu
wenye uwezo. Fimbo ya mbali haiui nyoka, kwa hiyo unaweza kufanya
lolote, naye hatakuwa na cha kufanya zaidi ya kumuachia machozi na
sononeko.
Kuna watu hawajiulizi hili; huyo anayekuja kwako akitumia fedha
kukuteka kwenye himaya yake, ameshatumia jeuri hiyo kwa wangapi? Endapo
utaujua ukweli, utakuja kufahamu kwamba ni wengi aliwanasa kwa sababu
alitanguliza fedha.
Weka akilini kwamba haji kwako kwa sababu anakupenda ila anayo jeuri
kuwa hutapindua kutokana na fedha alizonazo. Sasa basi, unapomkubalia
unamfanya aongeze kiburi. Kesho atatupa ndoano kwa mwingine na huo ndiyo
utakuwa mwendo.
Atakutamani kwa sababu ya muonekano wako, kwa hiyo kutokana na kiburi
cha fedha alichonacho, kesho akimuona mwingine atakayemtamanisha,
atatumia fedha zake kumnasa. Hii ina maana kuwa mkondo wako, watapita
wengi. Mwisho kabisa, utabaini kwamba uliingia katika msafara wa kenge.
Atapita kwa wenye tamaa za fedha, nawe utakuja kuingia humohumo. Hii
ndiyo sababu ya kusema utajikuta umeunga msafara wa kenge. Wewe utasema
unajiheshimu lakini huyo uliyeangukia kwake, hachagui.
Popote kambi, baadaye unapata jawabu kwamba umechangia mwanaume na machangudoa wengi wa mjini.
Tatizo siyo mvuto wako, wapo machangudoa wengi mjini na wanavutia
kwelikweli. Kama kavutiwa na wewe na katumia ngawira kukunasa,
inashindikana vipi kuvutiwa na machangudoa wengine, nao akatumia fedha
kuwanasa? Tena wao si gharama, kwa maana ndiyo kazi yao.
Vilevile kwa mwanaume, atampuuza mtu anayempenda na kumvaa mwingine
anayemuona anavutia zaidi. Wengi wamefanya hivyo bila kujua kwamba hao
wanaovutia barabarani, asilimia kubwa ni magubegube. Unahitaji mwandani
wa maisha yako, tuliza akili.
Sikukatazi kutupa ndoano, ila jaribu kufikiria mara mbili. Uliyenaye
hakutoshelezi? Kumuacha mpenzi wa kweli na kujishughulisha na wengine ni
sawa na mfano wa mtu aliyepoteza almasi, wakati alipokuwa ‘bize’
akitafuta mawe. Usilie kama wenzako, tuliza akili leo.
Kuna watu wanateseka leo. Wanadai wana mkosi. Eti, mapenzi
yanawachapa bakora kwamba hawana bahati nayo. Kama na wewe upo kwenye
kundi hili, fumba macho halafu ufikirie ulipotoka. Je, hukumuacha
aliyekupenda kwa dhati? Hukuchezea moyo wa yule aliyekuwa anakujali?
Kama jibu ni ndiyo, basi hutakiwi kulia. Mapenzi yalivyo, kupata
mwenye moyo mkunjufu katika kupenda ni bahati nasibu. Hivyo basi, kama
ulimchezea, ni zamu yako kuteseka kwa maana uliyachezea mapenzi.
Ulimpiga teke anayekupenda, sasa unahangaika na wasiokupenda.
Wanakuinjoi tu.
Pupa katika mapenzi inapunguza uwezo wa kufikiri

Kama kawaida tunaendelea na mada zetu, nimepokea malalamiko mengi
katika uhusiano, yanayotokana na mtu kupenda na kugeuzwa mtumwa wa
mapenzi na kupata mateso mazito.
Kwa nini unageuka mtumwa wa mapenzi?
Wengi wamekuwa wakiteswa na mapenzi kwa vile hawakuyasoma mwanzo,
matokeo yake huwa sawa na mtihani mgumu usiojua majibu yake, lazima
utafeli.
Mapenzi yanasomwaje?
Wengi huyachukulia mapenzi kama starehe na kusahau kuwa ni mwanzo wa
kujenga familia, tumekuwa tukiingia kwenye mapenzi kwa njia ya macho na
si kutumia akili.
Nina maana gani?
Binadamu tumeumbwa na tamaa, kila kiumbe kinapenda kitu kizuri, macho
huwa ya kwanza kuona na kupeleka taarifa kwenye moyo ambao nao
hulipokea jambo kama lilivyo na kulitaka kwa vile ni zuri, bila
kuangalia faida na hasara zake.
Hii hutokana na nini?
Siku zote pupa hupoteza uwezo wa kufikiri, hasa pale mtu anapoamini
kuwa kutaka kumjua kiundani mpenzi wako ni kupoteza muda, wengi huhofia
kuwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha umpoteze mpenzi wako na
akachukuliwa na mtu mwingine.
Kila mwanadamu anatanguliza tamaa ndiyo
upendo unafuata, wengi wetu huwa na pupa baada ya kumtamani mtu kwa
muda mrefu. Siku ukibahatika kumpata, pupa hutangulia mbele, hivyo
kufurahia bahati ile na kusahau katika mapenzi kuna kitu cha ziada.
Kweli
mapenzi ni bahati nasibu lakini bado tunatakiwa kupoteza muda kidogo
baada ya kumpenda mtu, lazima ujue historia yake, udhaifu wake kitu
ambacho kitakusaidia kurekebisha kabla ya kuingia katika uhusiano
kamili.
Wengi wetu tumeponzwa na pupa, tunakuwa kama samaki, hatufikiri, baada ya kuona chambo tunameza tu bila kujua madhara yake.
Watu
wa aina hii huja kushtuka wapo ndani ya uhusiano kamili, hivyo kubakia
kuteseka na kugeuka watumwa wa mapenzi, kila siku kulia na kujiona una
bahati mbaya kwa kulitupa penzi lako jalalani na kukosa heshima ya
mapenzi.
Siku zote mwanadamu ameumbwa akiwa na sifa kuu ya kufikiri
kabla ya kutenda na anayefikiri huwa hana pupa, hufikiri kwa kituo na
kupata jibu kuwa hili linafaa na hili halifai.
Hata kama uliyempata
alikuwa chaguo la moyo wako, kwa vile ulitanguliza pupa, sasa hivi
amegeuka chukizo la moyo wako, kila siku mateso ya upande mmoja. Kabla
ya kupenda jiulize unayempenda naye anakupenda?
Utamjuaje?
Uwe mkweli na muwazi, pia kuwa tayari kuishi maisha ya aina yoyote,
hamuwezi kuishi maisha ya furaha mkiwa na kitu tu na kama hakuna kitu
basi kero mtindo mmoja na kuiona nyumba yako kama mochwari.
Siku zote
kwa muda mfupi lazima utagundua vitu vingi kwa mpenzi unayetaka kuwa
naye kama udhaifu wake ambao utaufanyia kazi kabla ya uhusiano na kama
hawezi kubadilika basi hakufai, bado una kazi ya kumtafuta mwingine kwa
utulivu, acha pupa.
Fedha, uzuri si kinga ya mapenzi, kuna kitu cha ziada

WAKATI akili yangu ikianza kupata ufahamu, nilikuwa natatizika na
kuwaza kitu gani hasa katika mapenzi kinaweza kumfanya mtu atulie ndani
ya penzi lake. Niliamini kuwa na fedha ndiyo dawa ya mtu kumtuliza
mpenzi wake au kwa mwanamke kuwa mzuri na mwenye sifa zote, ndiyo dawa
ya kumfanya mpenzi wako atulie.
Baada ya kukua na kuingia katika dunia ya ufahamu wenye mitihani
mingi ya mapenzi, nimegundua kuna utofauti mkubwa katika vitu
nilivyoviwaza.
Wakati nakua, nilikutana na matukio ambayo niliona
kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano, lakini baada ya kupevuka,
nilipata majibu ya maswali yaliyonisumbua kipindi kile cha utoto.
Sikuamini
mke wa tajiri kufanya mapenzi na muuza mchicha, mwanaume mwenye mke
mzuri kutembea na changudoa au msichana wa kazi asiyejua kuvaa wala
kuoga.
Baada ya kuingia katika kazi hii ya kukumbushana mambo ya
mapenzi, nilipata maswali mawili ya watu wawili tofauti lakini yalikuwa
na jibu moja.
Mmoja alilalamika ana mke, anamhudumia kila kitu
ikiwemo familia yake lakini alichomlipa ni kutembea na mtu asiye na
mbele wala nyuma. Mwingine alilalamika kuhusu mpenzi wake kutembea na
mwanamke wa nyumba ya pili ambaye haufikii hata mguu wake kwa uzuri.
Kabla
ya kulizungumzia hilo, nirudi kwao kuwaeleza kukosa uamini hakuangalii
katembea na tajiri au mwanamke anayekushinda uzuri, kutoka nje ya
uhusiano au ndoa ni kosa kwa vile penzi ni la watu walioridhiana au
kuoana wakiwemo waliooa wake zaidi ya mmoja.
Leo nawajibu wote kuwa
fedha au uzuri wa mtu havibebi ndoa au uhusiano. Nimekuwa muumini mzuri
wa kuwaeleza penzi la kweli lipo vipi, mapenzi ni upendo wa dhati kutoka
moyoni, kuwa tayari kujilinda na kujiheshimu bila kujali una fedha au
ni mwanamke mzuri.
Mapenzi ni mbegu inayohitaji udongo wenye rutuba
ya upendo ili mbegu hiyo imee. Siku zote mwenye mapenzi ya kweli
humuangalia mtu, si kitu.
Tajiri na fedha zake asipopendwa huwa
katika mateso na kukonda wakati ana kila kitu. Penzi la kweli
halinunuliwi kwa gharama yoyote.
Tabia ya asili huwa sawa na moto
unaowaka kwenye pamba, ukitoa moshi ujue hakuna kilicho salama. Wapo
watu wasiokuwa na mapenzi ya dhati, utakuta mtu anajifanya anakupenda
ukiwa naye lakini mkiachana hana habari na wewe, hata kama mnakaa nyumba
moja na kulala kitanda kimoja.
Mtu anapoamua kutoka nje ya ndoa wakati ndani ana mke mzuri au mume wa ukweli anayempa kila kitu, kuna mawili:
Mosi:
Huenda mwanamke aliyenaye alimtamani kutokana na sura na umbile lake
na hakumpenda kwa dhati. Matokeo yake baada ya kumchoka, mwanamke
huonekana hafai na hukaa naye kimazoea.
Upande wa mwanamke, naye
huenda amekwenda kwa mwanaume kutokana na kujua ana fedha lakini anakuwa
hana mapenzi naye. Hapo lazima atatafuta penzi la nje ili afurahishe
nafsi yake, kwa hiyo watu hawa kutoka nje sishangai.
Pili:
Tabia ya kutoridhika na mpenzi mmoja, watu wa aina hii huwa
hawajisikii kula kitu cha aina moja kwa muda mrefu, lazima atatafuta mtu
wa kumfanya abadili mboga.
Vitu hivi vyote huwa vinawachanganya
watu, hasa wale wanaoamini kuwa mwanaume anapokuwa na fedha au mwanamke
anapokuwa mzuri, ni kila kitu katika mapenzi.
Mapenzi ni bahati, hasa
kumpata uliyemkusudia, basi muombe Mungu utakayemchagua naye awe kweli
amekukubali, hata ukiwa mbali kila mmoja amlindie mwenzake heshima, kwa
kutanguliza uaminifu mbele.
WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII
WANAUME
HUPENDA KUOA MWANAMKE WA AINA HII
Habari
za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na
nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada
mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku.
Wiki
hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa.
Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa
mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza
mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi
chote cha maisha.
Wanawake
wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata
wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie
wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali
sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura
nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao
nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa
nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika
mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo
ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.
MWEYE
MAPENZI YA KWELI
Lengo
kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na
ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya
ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli
bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu
kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio
kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. Mwanamke asiye na mapenzi ya
dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa
mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu
lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini
wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si
kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili
wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha
mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa
lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote
wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
Si
hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha
ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa
hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye
baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi
maisha ya raha mustarehe.
WENYE
TABIA NZURI
Tabia
njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni
katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu
cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo
wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani
utaambiwa anatabia mbaya. Naweza kusema
hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya
wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya
wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si
hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia
kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake
baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea
kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
WENYE
UCHU NA MAENDELEO
Hivi
karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi
hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa
hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za
kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa
wale ambao wako mijijini na hata vijijini. Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama
wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa
hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni
wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si
wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani
wafanye ili wafanikiwe.
WASIOPENDA
MAKUU
Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu
sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda
makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa,
kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?" Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki
tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia,
"mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali
kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na
usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

Wanawake
kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa.
Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na
pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda
lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia
akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’
hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani
ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume
ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho
watahitaji kama tu pesa haitakuwa
tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo
makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna
wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki,
anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine
wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.
Sisemi
kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba
ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano
wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa
na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha
ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
WAVUMILIVU
Wapo
wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku
zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio
wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni
za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume,
huyo siyo mwanamke wa kuoa.Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea
kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama
nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
Uvumilivu
kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza
hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na
atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya
starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
Licha
ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu,
wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo
kimsingi havikubaliki katka jamii.Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na
wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye
roho ya kwanini.
Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume
ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini
Dar-es-Salaam. Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue
kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa
umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza
yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza
kubadilika kwani inawezekana.
UKIPENDWA PENDEKA ILA USIPENDE SANA NA UWE TAYARI KUUMIZWA
MAPENZI! Hivi umeshawahi kukaa chini na kujiuliza kwamba, kama
yasingekuwepo mapenzi ulimwenguni binadamu wangeishi vipi? Kimsingi ni
swali gumu na hakuna anayeweza kulitolea jibu la moja kwa moja. Ni sawa
na wanaume wanavyojiuliza kwamba wasingekuwepo wanawake wangeishi vipi.
Ninachotaka kukizungumzia leo ni kwamba, mapenzi yamekuwa
yakiwasumbua walio wengi katika maisha yao hadi wengine kufikia hatua ya
kujilaumu kwa nini wameingia katika ulingo huo.
Wapo ambao
wamepoteza maisha kwa sababu ya mapenzi, wapo waliochanganyikiwa na
wengine kuathirika tu kisaikolojia kwa sababu ya mapenzi. Pia wapo
walioachishwa kazi kwa sababu ya mapenzi. Kimsingi mapenzi ni kitu
hatari sana kama hakitawekewa umakini.
Lakini sasa licha ya mapenzi
kuleta matatizo kwa binadamu, bado tunaambiwa kwamba, utakuwa peke yako
kwa muda fulani wa maisha yako na mwishowe utatakiwa kutafuta mwenza
ambaye utaishi naye kama mume na mke.
Swali la kujiuliza ni kwamba,
je kama kila unapoingia katika mapenzi unaumizwa na mtu ambaye umempenda
na ungetamani siku moja muoane, kuna ulazima wa kuendelea kung’ang’ania
penzi lake? Na kama utaendelea kuling’ang’ania penzi la mtu ambaye
anakuumiza kila wakati bila kujali, itakuwa inaleta maana?
Kimsingi
katika maisha ya sasa hasa kwa wale ambao bado hawajaolewa au kuoa,
wanatakiwa kuwa tayari kupenda na kupendwa lakini pia wanatakiwa
kutopenda sana kwani madhara yake ni makubwa. Pia wawe tayari kuumizwa
kwanza kabla ya kumpata yule mwenza mweye mapenzi ya dhati kwao.
Mapenzi
ya sasa yamejaa usanii wa hali ya juu kiasi kwamba ukifanya uchunguzi
utabaini wengi walio katika uhusiano wa kawaida yaani ‘boyfriend &
girlfriend’ wanapitisha muda tu lakini uwezekano wa wao kuja kuwa kitu
kimoja ni mdogo sana.
Unaweza kuwa katika uhusiano na mtu akawa
anakuonesha mapenzi ya kweli mpaka mwenyewe ukajiona mwenye bahati
lakini kumbe mwenzako anakufanyia usanii tu. Sasa utajuaje kwamba huyo
uliyenaye hana mapenzi ya dhati kwako? Hapo ndipo penye shughuli pevu na
ndiyo maana wakati mwingi tunajijengea imani tu. Tunaamini kwamba, kwa
sababu ya mambo anayonifanyia mpenzi wangu, ni lazima atakuwa ameniweka
moyoni mwake.
Tutambue tu kwamba mapenzi ya kujifanyisha hayawezi
kuchukua muda. Utadanganya leo, utadanganya kesho lakini ipo siku mpenzi
wako atabaini tu kwamba amedondoka katika penzi lisilo sahihi na hapo
ndipo yaweza kuwa mwisho wa penzi hilo la bandia.
Ninachotaka
kukushauri wewe msomaji wangu ni kwamba, unapotokea kuingia katika
uhusiano wa kimapenzi na mtu kwa lengo la kutaka kuoana kisha yeye akaja
kukuumiza kwa kukufanyia mambo mabaya, chukulia kwamba ni safari ya
kuelekea kumpata mwingine mwenye mapenzi ya dhati kwako.
Najua
utaumia sana lakini kutakuwa hakuna jinsi, kama yeye kaamua kukuacha
huna nafasi ya kulirejesha penzi lake kwako kwa hiyo unatakiwa tu
kukubaliana na hali halisi.
Ila sasa baada ya kuumizwa, hutakiwi
kukurupuka kutafuta mtu mwingie wa kujaza nafasi hiyo. Hiyo ni mbaya
sana kwani unaweza kujikuta unaingia tena katika penzi chungu kuliko
hata lililopita. Kaa chini jiulize, mpaka kufikia mpenzi wako kukuacha
ni wewe mwenye makosa au ni yeye?
Kama ni wewe lazima ujute kwanza
na kuwa tayari kubadilika. Lakini kama utabaini kwamba hukuwa na kosa
lolote bali uliyekuwa naye kaamua tu kukuumiza kwa sababu zake
anazozijua, hilo muachie Mungu, yeye ndiye atakulipa wewe na
aliyekutenda.
IWEJE ULAZIMISHE NDOA KWA MTU USIYE NA MAPENZI NAYE?

MAMBO vipi watu wangu? Natumaini kwamba mambo ni freshi na mnaendelea
vyema na majukumu yenu ya kila siku. Mimi ni mzima bukheri wa afya na
tunakutana tena kupitia safu hii lengo likiwa ni lile lile la kuwekana
sawa katika masuala kadhaa yanayogusa maisha yetu ya kimapenzi.
Wiki
iliyopita niliandika mada iliyokuwa inaeleza jinsi wapenzi wanavyoweza
kujifunza kutokana na kifo cha msanii maarufu, Steven Kanumba. Ni
matumaini yangu mmejifunza kitu na kubadilika itakuwa ni jambo jema
kwenu.
Baada ya utangulizi huo, nigeukie sasa kwenye mada yangu ya
wiki hii. Wakati flani huwa najiuliza kwa nini tunakuwa na wapenzi, kwa
nini mapenzi yakawepo? Kwa nini tunaoa ama kuolewa? Kwa nini baadhi ya
watu huamua kujinyonga baada ya kuachwa na wapenzi wao? Kwa nini mapenzi
yamekuwa sehemu ya maisha yetu?
Kwa nini mapenzi yameharibu baadhi ya maisha ya watu? Huwa najiuliza maswali mengi na kupata majibu mengi pia.
Kwa
vyovyote itakavyokuwa mapenzi ni sehemu ya maisha yetu na kwa hakika
maisha yetu hayawezi kukamilika bila kuwepo mapenzi. Ninapozungumza juu
ya mapenzi namaanisha yale yanayotoka moyoni mwa mtu mmoja kwenda kwa
mwingine.
Mapenzi hayo hukamilika baada ya wawili hao kuwa na hisia
sawa za mapenzi. Elewa kwamba kama upo katika uhusiano na mpenzi ambaye
hakupendi, yaani wewe peke yako ndiyo unayempenda, wewe ni mtumwa wa
mapenzi. Kama ndivyo, kwa nini ukubaliane na hali hiyo ambayo unaweza
kuepukana nayo?
Unadhani hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kukupenda
kwa mapenzi ya dhati na penzi hilo likawa kwa pande zote mbili tofauti
na ilivyo sasa? Inawezekana! Huna sababu ya kulazimisha penzi kwa mtu
ambaye unaona wazi kwamba hampendi.
Mapenzi ni nguzo ya maisha yetu,
kama ukifanikiwa kumpata mpenzi ambaye atakupenda na wewe ukampenda ni
wazi maisha yako yatakuwa yenye furaha isiyosimulika. Mapenzi yapo hivyo
na kama ukienda kinyume chake lazima utaumia.
Wakati mwingine
unaweza ukapendwa na mpenzi ambaye hujampenda, unadhani kuna ulazima wa
wewe kulazimisha kumpenda? Moyo wako umeshazungumza na wewe, umekuweka
wazi kuwa hauna mapenzi ya dhati kwa mtu huyo, kwa nini ujilazimishe?
Tatizo hili mara nyingi huwa kwa wanawake na hao hao ndiyo wamekuwa
wakiongoza kwa kutoa machozi pale wanapotendwa.
Anatokea mwanaume
anampenda sana, anapomtongoza anajikuta hampendi, anachokifanya ni
kumwambia kuwa atamjibu baadaye. Lengo la kumwambia hivyo ni kwa ajili
ya kujipanga na kufikiria. Mapenzi hayafikiriwi kiivyo ndugu zangu.
Kama
mtu unampenda, unapomuona tu siku ya kwanza, moyo wako utakuambia bila
kukuficha na utabaki wewe tu kufanya maamuzi sahihi. Hii ina maana kuwa
atakapokuambia anakupenda, huwezi kusubiri zaidi, hutakuwa na kitu cha
kusubiri, ni nafasi uliyokuwa ukiisubiria kwa hamu sana na lazima
utamkaribisha.
Tatizo lilipo
Baadhi ya wasichana wakitongozwa na mwanaume ambaye
anaona wazi kuwa hampendi, lakini akawa na mali au uwezo mkubwa kifedha,
huamua kumkubalia kwa lengo la kupata vitu vya mwanaume huyo.
Hufanya
hivyo akijidanganya kuwa atajifunza kupenda akiwa ndani ya uhusiano na
mwanaume huyo kitu ambacho hakipo katika ulimwengu wa mapenzi.
“Fedha
anazo, magari anayo, hata kama simpendi nitakwenda naye hivyo hivyo
mwisho wa siku penzi litajijenga lenyewe taratibu,” baadhi ya wasichana
huwaza hivyo. Baada ya wazo hilo kuingia akilini mwake, huwa hana muda
wa kusubiri zaidi, anakubali na wakati mwingine huweza kuingia katika
ndoa.
Madhara yake
Yapo mengi, lakini kubwa ni lile la kutokutosheka na
mpenzi wako uliyenaye. Anaweza akakupa kila kitu lakini ukakosa penzi la
dhati ambalo ndiyo msingi wa maisha. Unajua kama kuna mtu anakupenda na
wewe unampenda, unajihisi furaha na amani siku zote. Kinyume cha hivyo,
furaha utakuwa ukiisikia kwenye bomba tu.
Madhara makubwa zaidi ni
pale utakapojikuta ukiingia katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa
ajili ya kusaka penzi la dhati. Unajua kitakachotokea? Kama hutaleta
magonjwa ndani basi siku moja utafumaniwa, lazima utafukuzwa nyumbani
kwa mwanaume huyo na kama ana hasira, anaweza kukuua.
JAMBO LA MSINGI
Ushauri kwangu ni kwamba, kamwe usijaribu kuingia
katika mkumbo huu wa watu wanaoingia kwenye uhusiano na watu ambao
hawajawapenda.
Maisha yenyewe ni mafupi hivyo kuwa makini, fanya
maamuzi sahihi yahusuyo maisha yako ya kimapenzi kwa umakini wa hali ya
juu ili usije ukawa mmoja kati ya wanaolizwa na mapenzi na kuishia
kujuta kila siku.
WEWE UNAWEZA KUWA MCHAWI WA MAPENZI YAKO
WATU
wanaamini mno katika uchawi. Wanamaliza fedha kwa waganga wa kienyeji
wakiamini kwamba wamerogwa, hivyo wanatafuta ufumbuzi kutoka kwa
wataalamu wa mambo ya asili. Wapo wanaoita mambo ya Kiswahili.
Kwangu
napinga kuita hivyo kwa sababu nami ni Mswahili na kwa uzoefu wangu,
sisi Waswahili hatuna utamaduni wa kutegemea mitishamba kuamua hatma za
uhusiano wetu wa kimapenzi. Ila baadhi wapo, tena wengi haswaaa!
Shika
hili kwamba wewe mwenyewe pengine ndiye mchawi wa mapenzi yako.
Hujiulizi kwa nini wengine wanadumu? Ni vipi wenzi wengine
wanaheshimiana? Inakuaje kwako imekuwa kinyume? Siyo suala la upepo,
wakati mwingine ni kujitakia.
Kivipi mwenzi wako hakuheshimu? Ni
makosa gani ambayo wewe umefanya? Ukishapata majibu ya maswali hayo,
utaweza kujua faida za wewe kujitambua. Nakuasa ushike moja kuu kwamba
mapenzi ni nidhamu.
Yapo kama kioo, ukiyaheshimu nayo yatakuheshimu
na utayaona murua. Endapo utayachukulia kwa mzaha, nayo hayatasita
kukufanyia mzaha. Mwisho utakuja kugundua kwamba yanakutesa, ukifika
hapo usiache kukumbuka nawe ulivyoyatesa.
Baadhi ya watu wanaamini
mazoea ndiyo yanasababisha mapenzi kupungua au kuchokana. Hilo siyo
kweli hata kidogo, tena nakataa kwa herufi kubwa kwa sababu wapo mabibi
na mababu waliopendana tangu enzi hizo mpaka hivi sasa.
Mapenzi ni
kitu tofauti sana kwenye hii dunia na hata nje ya sayari, husababisha
mambo kwenda sawa au kuharibika, kuna baadhi ya vifo hutokana na
mapenzi, kuna magonjwa watu nwanaumwa kisa mapenzi.
Ukipata mpenzi
anayekuelewa, anakujali na anakupenda, hata dunia iwe ya tabu kwako kwa
kiasi gani, utaiona inasogea kama kawaida na maisha yanaendelea vizuri
tu, naamini hapo unakubaliana na mimi.
Lakini ukiumizwa kwenye
mapenzi au kutopata mtu wa kukujali, kutosikilizwa basi hata kama dunia
kwako ina raha, utaiona ni chungu na kama kwako dunia ni chungu tangu
awali halafu ukaja kuumizwa, ndio hapo watu wanapowaza na kufikiria
kujiua kwa sababu haoni hata umuhimu wa yeye kuishi.
Baadhi ya sababu zinazoweza kufanya mapenzi kupungua au mwenza wako kubadilika ni hizi;
1. KUTOSEMA KWELI
Katika
mapenzi uongo ni kitu kibaya sana, uongo wa aina yoyote ile ni mbaya
katika mahusiano yoyote yale na huweza kupunguza mapenzi ya dhati na
uaminifu kwa kiasi kikubwa hasa kama mmojawapo atagundua kuwa mwenzi
wake ni muongo, anamdanganya.
Wapo ambao wakigundua mpenzi wake ni
muongo wanauliza au kuongea nao ambacho ni kitu kizuri na siku zote
napenda sana kusisitiza suala la wapenzi kujadili vitu mbalimbali
vinavyotokea kwenye mahusiano yao, lakini wengine wanaamua kunyamaza au
kuacha kabisa.
2. KUTENGENEZA PENZI LA PEMBENI
Moja ya jibu
nililolipata kwa watu wengi niliojaribu kujadiliana nao mada hii
walisema kuwa, mahusiano mengine yanasababisha mapenzi kupungua,
inaumiza sana kugundua yule unayempenda kwa dhati ana mpenzi/wapenzi
wengine. Kubali au kataa, hii ni moja ya sababu kubwa zinazofanya
mapenzi kupungua au kuvunjika kabisa.
Kamwe usimuumize moyo
akupendaye kiukweli, usimfanye ajutie penzi lako,usimfanye anung’unike
kwa unayomtendea, ipo siku utahitaji mapenzi ya kweli kwa mwingine na
hutayapata, ukimuumiza ipo siku nawe utaumia, mapenzi ya kweli
yanawezekana kama kunakuwa na uaminifu.
3. UPUUZI
Hii pia
huchangia kwa kiasi kikubwa kupunguza mapenzi kama sio kuyamaliza
kabisa. Unapokuwa kwenye uhusiano jitahidi kumpenda mtu wako kwa hali
yoyote na usiwe na dharau kwake au hata kwa marafiki zake au ndugu zake
au hata wengineo. Hakuna mtu anayependa mtu mwenye dharau hata awe nani.
Hata kama mwenzi wako ana uwezo mdogo kuliko wewe, hiyo isiwe sababu ya
wewe kumdharau.
4.MSEMA HOVYO
Hakuna kitu kinachoweza
kumfanya mwenza wako kukukimbia au hata kukosa uaminifu na wewe kama
akija kugundua wewe ni mropokaji na huna ‘kifua’ hasa kwa yale mambo
ambayo ni ya chumbani na hayakutakiwa kutoka nje. Hakuna mtu anayependa
siri zake kutoka hadharani na huwa inaumiza sana kwenye mapenzi kumpa
mtu siri zako halafu yeye anaenda kusimulia.
Mambo mnayafanya mkiwa wawili tena ndani lakini kesho unaenda kusimulia kwa watu, si jambo la busara hata kidogo.
UKWELI KUHUSU KUPENDA, KUPENDWA NA KUPENDANA!

TUJADILI pamoja; Unafahamu nini kuhusu mapenzi? Najua majibu ni
mengi, kuna wengine watasema mapenzi ni kupendana...mapenzi ni hisia
kutoka kwa mtu kwenda kwa mwingine n.k. Kuna wakati nilishawahi
kufafanua maana ya mapenzi.
Ngoja niwaambie rafiki zangu. Kwa tafsiri
yangu, mapenzi ni hisia za ndani kutoka kwa mmoja kwenda kwa mwingine,
hisia hizi ili ziwe sahihi ni lazima zigongane ndipo neno UPENDO huanzia
hapo.
Kwa maneno mengine, wawili hawa lazima wote wawe na hisia sawa
ndipo wapendane. Tunapokuja kwenye mapenzi sasa, inawapasa watu hawa
wawe wa jinsia tofauti – mwanamke na mwanaume. Muunganiko wa wapenzi
hawa hulenga kujenga maisha ya pamoja. Upo hapo rafiki yangu?
Yes!
Mapenzi ni maisha. Kwa hakika maisha yetu hayawezi kukamilika bila
kuwepo mapenzi. Ninapozungumza juu ya mapenzi namaanisha yale yanayotoka
moyoni kabisa. Si maigizo.
Ikiwa upo katika uhusiano na mpenzi
ambaye hakupendi, yaani wewe peke yako ndiyo unayempenda, wewe ni MTUMWA
WA MAPENZI. Kama ndivyo, kwa nini uwe mtumwa?
Unadhani hakuna
mwingine ambaye anaweza kukupenda kwa mapenzi ya dhati na penzi hilo
likawa kwa pande zote? Inawezekana, huna sababu ya kulazimisha penzi kwa
mtu ambaye hakupendi!
Mapenzi ni nguzo ya maisha yetu, kama
ukifanikiwa kumpata mpenzi ambaye atakupenda na wewe ukampenda ni wazi
kuwa maisha yako yatakuwa yenye furaha na hakika utafurahia maisha yako
na huyo mwandani wako. Mapenzi yapo hivyo na kama ukijaribu
kuyabadilisha utaumia mwenyewe!
Wakati mwingine unaweza ukapendwa na
mpenzi ambaye hujampenda, unadhani kuna ulazima wa wewe kulazimisha
kumpenda? Moyo wako umeshazungumza na wewe, umekuweka wazi kuwa hauna
mapenzi ya dhati kwa mtu huyo, kwa nini ujilazimishe? Tatizo hili mara
nyingi huwa kwa wanawake zaidi!
Anatokea mwanaume anampenda sana,
anapomtongoza anajikuta kuwa hampendi, anachokifanya ni kumwambia kuwa
atamjibu baadaye! Lengo la kumwambia hivyo ni kwa ajili ya kujipanga na
kufikiria! Mapenzi hayafikiriwi ndugu zangu!
Kama mtu unampenda,
unapomuona tu siku ya kwanza, moyo wako hutetemeka juu yake na hutamani
uambiwe kitu fulani na huyo aliyeuteka moyo wako ghafla. Hii inamaana
kuwa atakapokuambia kuwa anakupenda, huwezi kusubiri zaidi, hutakuwa na
kitu cha kusubiri, ni nafasi uliyokuwa ukiisubiria kwa hamu sana, na
lazima utamkaribisha!
‘KUJITAHIDI KUPENDA!’
Baadhi ya wasichana, akitongozwa na mwanaume
ambaye anaona wazi kuwa hampendi, lakini akawa na mali au uwezo mkubwa
kifedha, huamua kumkubali kwa lengo la kupata vitu vya mwanaume huyo.
Hufanya hivyo ajidanganya kuwa ‘atajitahidi’ kumpenda taratibu akiwa
naye ndani ya uhusiano.
“Pesa anazo, magari anayo, hata kama simpendi
nitajitahidi kumpenda taratibu,” ni kauli ya kawaida sana kwa wasichana
ninaowazungumzia hapa.
Baada ya wazo hili kuingia akilini, huwa hana
muda wa kusubiri zaidi, anakubali na wakati mwingine huweza kuingia
hata katika ndoa.
NI HATARI KUBWA!
Kuna mengi ambayo yanaweza kutokea kwa
kujidanganya kuingia kwenye sehemu ambayo huna mapenzi nayo. Kubwa zaidi
ni ile hali ya kutokutosheka na mwenzi uliyenaye.
Anaweza akakupa
kila kitu lakini ukakosa penzi la dhati, ambalo ndio msingi wa maisha.
Unajua kama kuna mtu anakupenda na wewe unampenda, unajihisi furaha na
amani siku zote.
Madhara makubwa zaidi ni pale utakapojikuta ukiingia
katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa ajili ya kusaka penzi la
dhati! Unajua kitakachotokea? Kama si kuambulia kipigo, basi utafukuzwa
nyumbani kwa mwanaume huyo. Yote hayo ya nini?
BAKI NA HILI
Kamwe usijaribu kuingia katika mkumbo huu, mkumbo wa
kuingia kwenye uhusiano ukiwa na uhakika huna mapenzi ya dhati. Ni jambo
gumu ambalo huweza likaharibu maisha yako kabisa.
Tambua thamani ya
mapenzi kwa kuheshimu hisia zako za ndani. Unapoamua chochote kuhusu
mapenzi ujue unaamua jambo linahusu maisha yako.
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi anayeandikia
magazeti ya Global Publishers. Ameandika vitabu vya True Love, Let’s
Talk About Love na Who is Your Valentine vilivyopo mitaani.
ATHARI ZA KUFANYA MAPENZI MARA KWA MARA

Wapenzi
wengi hasa wale ambao uhusiano wao ni mchanga hupenda sana kufanya
mapenzi kila wanapokutana au wanapohisi wamehemkwa na miili yako.
Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi
kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata
matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana
ngono.
Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.
Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta
kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa
kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa
mahari.
Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa
upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya
watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la
watu wapenda ngono.
Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara
mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa
anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa
kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana
hata kwenye nguzo ya umeme na chini ya miti kwa vile tu miili imetaka
kufurahika.
KUPOTEZA HAMU YA TENDO
Watu
wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa
wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza
wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara.
Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.
Aidha
kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na
kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu
moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya
mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu
naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.
KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA
Tabia
ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini
na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa
tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye
uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi
na kwa wakati gani
Watu
wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao
kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake.
Hawa ndiyo
wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya
mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika
kwa tamaa ya mapenzi.
Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.
KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO
Raha ya tendo hutegemea sana hisia
iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo
basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko
wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa
yako.
Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!
KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI
Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili.
Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke.
Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.
Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.
KUPATA MAGONJWA
Kama tulivyojifunza kuwa watu
wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya
mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo
ukimwi.
Ufanyaji wa
mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya
waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza
kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia
michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa
ukiwemo ukimwi.
Baada ya kungalia madhara hayo
machache ni vema kwa wapenzi kupunguza kiwango cha kufanya mapenzi ili
kuifanya miili iwe na uvumilivu unaoweza kumsaidia mtu kukaa kwa muda
mrefu bila kumsaliti mpenzi wake hata kama atakuwa amesafiri mbali naye
kimasomo, kikazi au kibiashara.
Makosa katika mapenzi..
KUNA watu wanaanzisha mapenzi, kabla ya yote
tayari wanazungumza kwamba katika uhusiano wetu tutakuwa hivi na vile,
lakini kuna mwingine unamwambia tu unampenda, dakika tano zijazo tayari
mnakwenda kukutana faragha.
Wapo watu hawajihurumii kufanya mambo kama haya pasipo kujiuliza huyu ninaye ili awe nani.
Kuna wengine ngono wanaona kama kwenda haja ndogo na kurudi, si suala
linalohitaji staha au mazungumzo ya kina kuhusu hatma yenu.
Je wewe ukoje? Ni vizuri kujiheshimu. Usijirahisi, onyesha msimamo.
Usiwe mwepesi kuugawa utu wako ili umfurahishe huyo uliyenaye.
Wengine wanatoka kwao wakijua kwamba wana wapenzi, lakini wakifika
sehemu za kazi, wanajirahisi, huyu akimtaka anakubali, hana msimamo,
haya si maisha. Kama huyu mfanyakazi mwenzako, bosi wako anakutaka, je,
kawataka wangapi? Hili ni jambo la kujiuliza.
Wengi kati ya watu wa aina hii huachwa kwa visa. Ni kwa sababu wanaonekana ni watu wasio na misimamo kwa hiyo humthamini.
Mnaweza kuachana kwenye nyumba ya wageni, au unaweza siku unampigia
simu mwenzi wako mliyekubaliana mkutane sehemu fulani, haji kwa wakati.
Ni kwa sababu anakuona hufai.
Haiwezikani mwanamke kweli mwenye kujiheshimu, unamtongoza saa moja na nusu, saa mbili kamili mko kwenye nyumba ya wageni.
Tena wengine unaweza kuanza kwanza kutafuta sehemu ya kumpeleka kabla
ya kumhitaji, ni kwa namna tu anavyoonekana hajijali utu wake.
Kuna simulizi moja ni ya kweli, dada mmoja mrembo alikwenda baa kunywa,
akakukatana na mwanamume, wakazungumza na kukubaliana waende nyumba ya
wageni siku hiyo, lakini wakiwa chumbani mwanamke alidanganya
anakwenda chooni, hakurudi, alikimbia.
Simulizi nyingine inahusu msichana aliyetongozwa na kujibu kuwa
anachohitaji yeye ni mtu ambaye atakuwa mume na yeye awe mke? Aliendelea
na msimamo huo hata baada ya kubembelezwa sana.
Je, kama wewe ni mwanamume ungeoa yupi kati ya hawa? Katika hali ya
kawaida, mwenye busara angeoa huyu ambaye ameshikilia msimamo. Kwa
sababu ni wazi hata baada ya kuoana atakuwa na msimamo.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa wengi wanaachana kwa visa kwa sababu
anaona hana njia nyingine hasa kwa sababu labda anang�ang�aniwa na mtu
ambaye hakuwa na sifa.
Japo watu wengine wanaachana labda kwa sababu amepata mwingine, lakini
walio wengi wanaachana baada ya kubaini kuwa fulani hamfai.
Wengine pia huachana kwa sababu tu amepata mwingine, ambaye anaamini ni
bora zaidi, ingawa wakati mwingine baada ya kujuana kwa kina, anaweza
kuwa ni mbaya zaidi ya yule aliyetaka kumuacha.
Ndugu, kama ambavyo huyo uliyenaye zamani ulikuwa ukimuona mzuri na
sasa unamuona mbaya, huwezi kujua kuhusu huyu ambaye unataka kuwa naye
baada ya kumuacha huyo wa sasa.
Ndipo huwa nashauri kuwa wakati mwingine kama uliyenaye si mbaya sana,
ni vizuri mkaendelea kuwa naye. Mambo yanaweza kurekebishika na kuwa
safi.
Fanya hivi hasa kama rekodi yake haionyeshi kuwa ni mtu mbaya, mfano
kama mtu aliwahi kuwa na mke au ana mtoto lakini hamjali, huyo kama
umeoana naye na ikatokea mmeachana, ni makosa makubwa kurudiana naye.
Dalili zinaonyesha ni mtu asiyefaa, ni vigumu kuishi vizuri hata kama mtarudiana.
Kimsingi ni vigumu kuishi vizuri na mtu ambaye tayari mliachana kisha mkarudiana.
Tafiti nyingi kuhusu jambo hili zinaonyesha kwamba ni vizuri kama
tayari mmeachana na mtu, kila mmoja akaendelea na hamsini zake.
Wengi wa wale wanaorudiana hali ya mahusiano yao huwa ni mbaya zaidi ya
zamani, hasa baada ya miaka miwili tangu kurudiana kwao. Kama ni visa
huwa ni zaidi.
Ninachotaka kusisitiza katika mada hii ni kwamba haijalishi una
mwingine anayekushawishi kuachana na huyo wa sasa, au humtaki tu fulani,
ni vizuri kuachana pasipo visa.
Hakuna sababu ya kuanza kumtangaza huyo mwenzi wako vibaya kwa watu ili
tu aonekane ni mbaya, wakati pengine si mbaya, ila unataka kuachana
naye kwa sababu zako.
Ndugu zangu hapa duniani tunapita, hakuna sababu ya kutendeana mambo
mabaya. Jitahidi kuwa wazi, mwambie ukweli kwamba kweli nilikupenda,
lakini hatuwezi tena kuwa pamoja kwa sababu hizi na zile.
Ni kweli ataumia, lakini ipi ni bora kuendelea na visa, au kumueleza
wazi ajue moja, kama ni maumivu ya mara moja, iko siku yataisha. Ni
vizuri kuelezana ukweli.
Lakini jambo moja la kujua ni kwamba ikiwa unamuacha mtu kwa sababu tu
ya kumnyanyasa, hana kosa lolote, unaweza kupata mtu ambaye atakuja
kuwa mbaya kuliko yule ambaye umemuacha kwa kumuonea wakati anakupenda.
Kuacha mpenzi kwa sababu zisizo na maana, ni kujitafutia laana.
Ili kuepukana kuachana ni vizuri kabla ya kuanzisha uhusiano kujuana kwa kina, ridhika na nafsi yako kabla ya kuamua.
Zungumzeni kuhusu dini, maana wengine wanakaa weee baada ya muda ndipo
wanaanza kusema, eeeh bwana dini yetu si moja, ndugu wamekataa
tusioane. Siku zote mlikuwa wapi kuzungumzia hili?
Unahitaji mwenzi wa kufa na kuzikana? Soma muongozo huu
Ni njia gani za kumpata mwenzi wa maisha yako? Inawezekana unakabili
mtihani mzito, hujui ni yupi wa nafsi yako. Bila shaka unamtaka yule
wako wa kufa na kuzikana.
Mada hii inakuja na suluhisho mahsusi kwako, kumjua mapema anayekufaa,
anayeweza kudumu nawe maishani. Zingatia kwamba mwenzi sahihi wa maisha
yako ni hatua muhimu kuelekea kwenye mafanikio.
KWANZA TAMBUA HILI
Uhusiano wa kimapenzi ni suala binafsi. Kwanza kabisa ni sanaa
inayokutaka uangalie mahitaji yako mwenyewe. Je, unahitaji nini kwa mtu
ambaye ungependa awe mwenzi wa maisha yako?
Yale unayotaka kutoka kwa mtu ambaye unapenda awe mwenzi wa maisha
yako, unapaswa kuyapa kipaumbele. Hata siku moja, usithubutu matamanio
ya mwili na moyo yakupe mwongozo wa kumwona umpendaye.
NANI MWENZI WA MAISHA?
Ni swali ambalo unapaswa kujiuliza. Kwa uwazi kabisa, unatakiwa
kuzingatia kuwa mwenzi wa maisha ni yule ambaye utachangia naye mambo
mengi kwa uaminifu na maelewano makubwa.
Mwenzi wa maisha si mtu unayeweza kuwa naye kwa mantiki ya kupeana
tulizo la ngono unapohitaji au kampani ya kwenda kuangalia ‘muvi’,
muziki, ufukweni na kwingineko unapoona huhitaji kuwa peke yako.
Mwenzi wa maisha ni yule atakayefanya ujione umekamilika, bila kujali
‘ubize’ wala ukapa ambao pengine unao ndani ya jamii inayokuzunguka.
Kingine cha kuzingatia ni kwamba, mwenzi wa maisha yako ni yule ambaye
anakukubali na kukupenda kama ulivyo, bila kuwepo kwa nyongeza ambazo
zitatokana na kukubadilisha kutoka yule wa zamani.
Kupata mwenzi wa maisha mwenye sifa kamili, ni sawa na kupatia herufi
ya mwisho kwenye mchezo wa kubahatisha. Kwa maana hiyo, baada ya
kumpata, kila kitu kinakuwa kimekamilika maishani mwako.
NANI MWENZI WA MAISHA YAKO?
Pointi ya msingi kuzingatia ni kwamba unahitaji kuwa na yule
anayekubalika ndani ya nafsi yako. Hivyo basi, fikiria kwa yale
yanayoweza kukufanya uwe na furaha, pia yanayoweza kukupa huzuni.
Zingatia mapitio yako ya nyuma kuona ni kwa namna gani yamekutengeneza
mpaka kufika ulivyo sasa. Jiulize pia kuhusu ndoto na malengo yako siku
za usoni.
Ikiwa tu utaweza kutambua mahitaji na matarajio yako ya kimaisha, bila
shaka utaweza kutambua ni mtu gani anayefaa katika kukusaidia kutimiza
kila kilichomo ndani ya malengo yako.
JENGA IMANI
Kutafuta mwenzi wa maisha siyo suala la kuangalia mtu wa kwenda naye
klabu kujirusha usiku. Vile vile ni muhimu kutambua kwamba inaweza
kukuchukua muda kupata mtu wa kukidhi vigezo vyako.
Pamoja na ukweli huo, bado unatakiwa uwe na imani kwamba itafika wakati
utasahau habari za kutafuta mwenzi na utakuwa mwenye furaha,
ukijipongeza kwa kumpata anayekufaa.
Mapenzi ni mchezo lakini ni rahisi kuucheza ukitambua kanuni zake. Hii
ina maana kuwa unapokuwa kwenye kipengele hiki, unakuwa na jukumu moja
zito la kuhakikisha unampata yule mwenye uwezo wa kukonga moyo. Mwenye
sura ya kutimiza malengo yako.
Hata hivyo, muhimu kwako ni kuwa mtulivu na kuacha macho yafanye kazi
ya kuangaza kwa utaratibu, halafu akili ifanye kazi ya kutathmini
kiwango cha huyo atakayeonwa.
Kitu kingine ambacho unatakiwa kuheshimu ni kuwa, wawili wanaopendana,
kila mmoja kwa nafasi yake ni nusu ya kitu kizima kinachoitwa ndoa au
wapenzi, hivyo wanapounganishwa ndiyo kinapatikana kitu kizima.
Ukiamini kuwa wewe ni nusu na utakamilika baada ya kukutana na mwenzi
wako, unachotakiwa kufanya ni kujenga imani kwamba mwenzi wako yupo
sehemu kwa ajili yako, hivyo endelea kumtafuta na siku moja utamuweka
mikononi mwako.
Dalili 10 za mwanaume anayekupenda.
ANAVYOTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani
aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana
kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50.
Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama
msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa
kuacha kumwangalia, ujue anampenda.
MIPANGO
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda
mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na
pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo.
Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini
kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.
ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye
upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa
mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha.
ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa
ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake,
atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi
yake.
ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na
kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya
kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako
kuonekana wakati wote chumbani kwake.
UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi
wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao
vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa,
kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.
ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda
atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua
wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.
ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda
atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa
unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa
maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya
nyumbani.
ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na
kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna
mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa
tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume
anayekupenda kwa dhati.
ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na
wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda
atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na
kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.
Mada hii inaishia hapa, hebu jiulize mwanadada, huyo uliyenaye
anakufanyia haya, kama sivyo kwa kiwango kikubwa utakuwa na kazi ya
kuhakiki penzi lako na pengine kujenga misingi mipya ya uhusiano wenu
kabla haujavunjika.
NJIA SAHIHI ZA KUACHANA NAMWENZI WAKO
Unapotaka kupeleka ujumbe kwa mpenzi wako kuwa hayuko tena moyoni mwako,
lazima tu ujitolee kupata hasara katika baadhi ya mambo. Kumbuka kuwa
huhitaji tena uhusiano na mwenzako.
PUNGUZA MWITIKIO WAKE
Kuna wakati ambapo rafiki au mpenzi wako atafanya au kusema jambo na
wewe utatakiwa kuonesha mwitikio. Kama umeshadhamiria kuachana naye,
onesha mwitikio wa shingo upande.
Kama mhusika atabaini jinsi ulivyoitikia shingo upande, utakuwa
umepeleka ujumbe maridhawa, kuwa huna tena furaha na uhusiano wenu na
kwamba unahisi ni wakati muafaka wa kumaliza mambo.
Kuna mazingira ambayo hutaepuka kumwitikia mpenzi au rafiki unayetaka
‘kumpiga chini’. Kwa sababu hiyo, ndiyo maana unapaswa kumwitikia lakini
katika hali ambayo inaonesha kwamba huna habari naye tena.
Unapomwitikia mpenzi wako kwa shingo upande, unamwonesha kuwa yeye siyo
kipaumbele kwako, jambo ambalo litamfanya kuona kuwa yamkini ni wakati
muafaka wa kupunguza moto wake kwako.
PUNGUZA UKARIBU NAYE
Kama umekuwa na mazoea ya kuwa karibu na mpenzi wako kama ilivyo
kawaida, anza kujenga mazingira ya kujitenga naye mnapokuwa mbele za
watu ili aweze kuhisi mabadiliko katika mwenendo wako.
Haina maana kuwa usizungumze naye, kaa naye karibu na uzungumze naye
kama kawaida, lakini majibu yako yawe ya mkato. Pia usikae karibu naye
sana, maana namna hiyo utalazimika kuzungumza naye na kukaribisha
lugha yake ya matendo.
Lakini kama itawezekana, jishughulishe zaidi kuzungumza na watu wengine
ili kwa kiasi fulani huyo mwenzako aweze kuona kuwa hukumpa kipaumbele
cha kwanza.
ONESHA WATU KWAMBA HAUPO NAYE
Bila kulazimika kumfedhehesha mwenzako, chukua hatua za kuuonesha umma
unaowazunguka kuwa yeye si tena mdau muhimu katika maisha yako,
mathalani kwa kutomwalika kwenye shughuli muhimu ambazo ulizoea
kumwalika.
Unapolazimika kumwalika, weka mipaka katika mazungumzo yako na yeye.
Hata hivyo, haishauriwi kuwatangazia marafiki zako wengine kuwa unataka
kumtenga mpenzi au rafiki yako huyo, maana namna hiyo watajiwa na
fikra kuwa yamkini ana matatizo kumbe kwa hakika kama kuna mwenye
matatizo basi ni wewe (au unavyopaswa kuwafanya watu waamini).
Kama unataka kuwa mstaarabu, hakikisha kuwa hakuna mtu mwingine
anayeingia katika mchakato huu wa kumbwaga mpenzi au rafki yako, kwani
hii ni suala lako binafsi.
USIJIBEBESHE MZIGO
Hakuna haja ya kubeba mzigo wa uhusiano ambao huna maslahi nao. Japo
baadhi ya wanawake huwalalamikia wanaume ambao huwachezea kisha
wakawaacha, ukweli ni kwamba hupaswi kuendelea na uhusiano ambao
haukupi kile ukitakacho.
Watu wengi walishafanya hivi na kufanikiwa kumaliza vema uhusiano wao
na wapenzi wao. Hakuna ubaya wowote kufanya hivi pale unapoona kuwa
mwenzako anakupeleka kule ambako usingependa kwenda kwa sasa.
Iwapo utatokea mgogoro wowote au mpenzi wako akawa na malalamiko,
bahati nzuri tayari unazo sababu zako ambazo umetakiwa kuziweka bayana
mawazoni.
Hapo ndipo utakapozianika mbele yake na kumweleza msimamo wako mpya.
Hata hivyo, utaratibu huu wa kumaliza uhusiano unafaa zaidi kwa wapenzi
ambao mahusiano yao hayajajenga mizizi au wale ambao ni marafiki wa
kawaida.
Kama uhusiano wako na mwenzako umeshaota mizizi, zipo tahadhari nyingi
zaidi za kuchukua, maana ulishampotezea mwenzio muda mwingi.
fanya haya! Unapotokea kumpenda mtu aliye na mpenzi wake,.
Tumshukuru
Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa
wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi.
Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya
kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila
mtu.
Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa,
utabaini nyuso zao zimetawaliwa na furaha isiyo na kifani. Lakini
mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.
Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii
la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika
kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.
Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara
kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia
mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.
Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa
kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa
akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.
Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta
mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa
demu ambaye tayari ana mpenzi wake.
Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?
Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au
utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake?
Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo
huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi
kwako.
Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.
Chunguza
Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao
umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa
sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu
na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema
chunguza uhusiano wake kwanza.
Usitafute uadui
Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta
subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini
kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui
bure, kaa pembeni.
Una nafasi kwake?
Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza
kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za
kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa
mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea
hautakuwa na nafasi.
Ni rahisi kubadili uamuzi wake?
Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha
huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea
naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.
Pingana na moyo wako
Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa
unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati
mwingine utakuwa unakupotosha.
Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye
mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya
kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.
Urafiki ni poa?
Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini
imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake
kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila
angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate
nafasi hiyo.
Usiumie, yupo mwingine
Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini
uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu
wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe
kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya
furaha.
Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani,
pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza
kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo,
usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!
Mambo ya kuzingatia unapomtumia mpenzi wako zawadi
Nazungumzia ishu ya wapenzi kununuliana zawadi. Hapa sizungumzii zawadi
ambazo wengi wetu tumekuwa tukinunuliana siku za Sikukuu kama vile
Iddi, Krismasi, Valentine na nyinginezo bali namaanisha zawadi nje ya
siku hizo.
Kumtumia mwenzi wako zawadi ni kati ya mambo ambayo humfanya afurahie
uhusiano wake na wewe. Hata hivyo, hakuna zawadi za moja kwa moja
ambazo ni rasmi kwa ajili ya wapenzi lakini ni vyema ukamtumia zawadi
kulingana na mapenzi yake zaidi.
Kwa kuwa wewe unamfahamu zaidi mwenzi wako, unaweza kujua zawadi gani
ni nzuri zaidi kwake au anayopendelea kuliko aina nyingine.
Wiki hii nimechambua aina kuu za zawadi ambazo ukimtumia mpenzi wako utamteka hisia zake na ataona unamjali.
Mavazi
Mavazi ni kati ya zawadi ambazo zitamfanya mpenzi wako azidi kukupenda na kuwa karibu zaidi na wewe.
Aina ya nguo ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ni zile ambazo
unaamini atavutiwa nazo au zile ambazo zitampendeza na kumfanya
aonekane nadhifu.Hata hivyo, zipo aina za mavazi ambazo zimependekezwa
zaidi kwa ajili ya wenzi kutumiana wanapokuwa mbali na hata wanapokuwa
karibu.
Kama wewe ni mwanamke unataka kumtumia mpenzi wako wa kiume, mavazi
yafuatayo yanafaa zaidi. Saa nzuri ya mkononi, nguo za ndani, lakini
lazima uzingatie rangi ya bluu, bluu bahari au nyeupe kimsingi zisiwe za
rangi zinazoficha uchafu.
Zingine ni fulana za ndani ‘singlendi’, fulana, mkanda wa suruali, simu
ya mkononi, vitambaa vya jasho n.k. Hakikisha katika zawadi hizo,
unaambatanisha na manukato mazuri hasa yale ambayo unajua atayapenda.
Haishauriwi kumtumia suruali au shati kwa sababu inaweza kuwa kubwa au
ndogo, hivyo kupunguza ladha ya zawadi hasa kama atakuwa ameipenda
sana.
Zawadi za aina hiyo, unaweza kumpa mwenzi wako ofa ya kwenda kuchagua
moja kwa moja dukani lakini kama unajua saizi yake na una uhakika
akivaa atapendeza, ruksa kumnunulia vitu hivyo na tena utakapopatia
saizi yake vizuri ataamini uko makini naye na unampenda kwa dhati.
Kama wewe ni mwanaume na unataka kumtumia mpenzi wako wa kike zawadi,
lazima uwe makini sana! Mavazi yaliyopendekezwa hapa ni pamoja na
batiki (gauni, blauzi na sketi, blauzi yenyewe n.k), hereni, bangili,
mkufu, simu ya mkononi, saa ya mkononi, nguo za ndani (kulingana na
mapendekezo yake, kwa jinsi umjuavyo), sidiria, viatu n.k.
Kama umesoma vizuri utaona mwanamke anaweza kununuliwa vitu vingi zaidi
(hasa nguo) tofauti na mwanaume. Hii inatokana na aina za mavazi na
saizi zao kukaririka kirahisi zaidi au kutokuwa na saizi ya moja kwa
moja. Mathalan, batiki, sketi na blauzi na vinginevyo. Kama kawaida,
mavazi haya, ambatanisha na manukato mazuri, hasa yale ambayo ndiyo
anayopendelea mpenzi wako.
Maua pia ni kati ya zawadi zinazopendekezwa na wataalamu wa mambo ya
mapenzi. Maua ni mazuri sana kwa mwezi aliye mbali, lakini ni vyema
kuzingatia na umbali uliopo kati yenu, kwani maua huweza kusinyaa kabla
ya kumfikia (hasa kama ukimtumia yale halisi, kwani ndiyo haswa
mazuri).
Hata hivyo, zipo zawadi nyingine ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kwa kuangalia vitu anavyovipenda sana.
Hii ni njia pekee ya kuonesha ubunifu wako na jinsi unavyomjali hata
akiwa mbali kwa kumtumia vitu ambavyo huwa anavipenda lakini alipo
hawezi kuvipata!
Mathalan, mpenzi wako anapenda sana zabibu lakini amekwenda mkoa ambao
vitu hivyo havipatikani kwa urahisi, hii ni nafasi yako kumtumia.
Mathalan unajua kabisa anapenda sana kusoma vitabu lakini sehemu
aliyopo hawezi kupata, basi nunua majarida, magazeti na matoleo yote
ambayo hajayapata kisha mtumie, hakika utakuwa umemfurahisha sana na
kumfanya afurahi kupata vitu hivyo.
Kwa leo naomba niishie hapo, lengo ni kukufahamisha kwamba zawadi ni
kitu muhimu sana katika kuliboresha penzi lenu. Kwanza mpenzi wako
aamini kwamba unampenda lakini pia unamjali.
Nazungumzia ishu ya wapenzi kununuliana zawadi. Hapa sizungumzii zawadi
ambazo wengi wetu tumekuwa tukinunuliana siku za Sikukuu kama vile
Iddi, Krismasi, Valentine na nyinginezo bali namaanisha zawadi nje ya
siku hizo.
Kumtumia mwenzi wako zawadi ni kati ya mambo ambayo humfanya afurahie
uhusiano wake na wewe. Hata hivyo, hakuna zawadi za moja kwa moja
ambazo ni rasmi kwa ajili ya wapenzi lakini ni vyema ukamtumia zawadi
kulingana na mapenzi yake zaidi.
Kwa kuwa wewe unamfahamu zaidi mwenzi wako, unaweza kujua zawadi gani
ni nzuri zaidi kwake au anayopendelea kuliko aina nyingine.
Wiki hii nimechambua aina kuu za zawadi ambazo ukimtumia mpenzi wako utamteka hisia zake na ataona unamjali.
Mavazi
Mavazi ni kati ya zawadi ambazo zitamfanya mpenzi wako azidi kukupenda na kuwa karibu zaidi na wewe.
Aina ya nguo ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ni zile ambazo
unaamini atavutiwa nazo au zile ambazo zitampendeza na kumfanya
aonekane nadhifu.Hata hivyo, zipo aina za mavazi ambazo zimependekezwa
zaidi kwa ajili ya wenzi kutumiana wanapokuwa mbali na hata wanapokuwa
karibu.
Kama wewe ni mwanamke unataka kumtumia mpenzi wako wa kiume, mavazi
yafuatayo yanafaa zaidi. Saa nzuri ya mkononi, nguo za ndani, lakini
lazima uzingatie rangi ya bluu, bluu bahari au nyeupe kimsingi zisiwe za
rangi zinazoficha uchafu.
Zingine ni fulana za ndani ‘singlendi’, fulana, mkanda wa suruali, simu
ya mkononi, vitambaa vya jasho n.k. Hakikisha katika zawadi hizo,
unaambatanisha na manukato mazuri hasa yale ambayo unajua atayapenda.
Haishauriwi kumtumia suruali au shati kwa sababu inaweza kuwa kubwa au
ndogo, hivyo kupunguza ladha ya zawadi hasa kama atakuwa ameipenda
sana.
Zawadi za aina hiyo, unaweza kumpa mwenzi wako ofa ya kwenda kuchagua
moja kwa moja dukani lakini kama unajua saizi yake na una uhakika
akivaa atapendeza, ruksa kumnunulia vitu hivyo na tena utakapopatia
saizi yake vizuri ataamini uko makini naye na unampenda kwa dhati.
Kama wewe ni mwanaume na unataka kumtumia mpenzi wako wa kike zawadi,
lazima uwe makini sana! Mavazi yaliyopendekezwa hapa ni pamoja na
batiki (gauni, blauzi na sketi, blauzi yenyewe n.k), hereni, bangili,
mkufu, simu ya mkononi, saa ya mkononi, nguo za ndani (kulingana na
mapendekezo yake, kwa jinsi umjuavyo), sidiria, viatu n.k.
Kama umesoma vizuri utaona mwanamke anaweza kununuliwa vitu vingi zaidi
(hasa nguo) tofauti na mwanaume. Hii inatokana na aina za mavazi na
saizi zao kukaririka kirahisi zaidi au kutokuwa na saizi ya moja kwa
moja. Mathalan, batiki, sketi na blauzi na vinginevyo. Kama kawaida,
mavazi haya, ambatanisha na manukato mazuri, hasa yale ambayo ndiyo
anayopendelea mpenzi wako.
Maua pia ni kati ya zawadi zinazopendekezwa na wataalamu wa mambo ya
mapenzi. Maua ni mazuri sana kwa mwezi aliye mbali, lakini ni vyema
kuzingatia na umbali uliopo kati yenu, kwani maua huweza kusinyaa kabla
ya kumfikia (hasa kama ukimtumia yale halisi, kwani ndiyo haswa
mazuri).
Hata hivyo, zipo zawadi nyingine ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kwa kuangalia vitu anavyovipenda sana.
Hii ni njia pekee ya kuonesha ubunifu wako na jinsi unavyomjali hata
akiwa mbali kwa kumtumia vitu ambavyo huwa anavipenda lakini alipo
hawezi kuvipata!
Mathalan, mpenzi wako anapenda sana zabibu lakini amekwenda mkoa ambao
vitu hivyo havipatikani kwa urahisi, hii ni nafasi yako kumtumia.
Mathalan unajua kabisa anapenda sana kusoma vitabu lakini sehemu
aliyopo hawezi kupata, basi nunua majarida, magazeti na matoleo yote
ambayo hajayapata kisha mtumie, hakika utakuwa umemfurahisha sana na
kumfanya afurahi kupata vitu hivyo.
Kwa leo naomba niishie hapo, lengo ni kukufahamisha kwamba zawadi ni
kitu muhimu sana katika kuliboresha penzi lenu. Kwanza mpenzi wako
aamini kwamba unampenda lakini pia unamjali.
HAWEZI KUSEX MPAKA ASHIKE UUME
Mimi ni msichana nimewahi kuwa na rafiki wa kiume hapo nyuma, huyo kaka
alikua tu kama rafikiyangu baadae ikatoke tukapendana na kuwa mtu na
girlfriend wake I mean tulianza kutoka kama wapenzi.
Huyo mwanaume alikua yuko nice ingawa baadae tulikuja tukaachana. Tatizo la huyo mwanaume ni wakati wa kufanya mapenzi.
Tulikua
tukifanya romance , tukiwa tunajiandaa kufanya mapenzi alikua yuko
vizuri , tu tunaendana vizuri na wote tunakua tuko tayari kungonoka ila
wakati wa kungonoka ndo kasheshe linaanzia hapo.
Kwanza uume wake hauingii, yaani ni
lazima ashikilie na mkono ndo aanze kuingiza na kutoa na hata kama
akishikilia bado hawezi kutia kabisa yaani hawezi kwenda juu na chini
na hata mimi nashindwa kumsapoti kukatika kwani uume wake unakua kama
umeshasinyaana.
Kitu
kingine alikua anadai eti uchi unateleza kwa hiyo ananifuta ndio
aingize ukiwa mkavu kabisa wakati mimi najua uchi ukiwa una ute ndio
rahisi kwa kufanya mapenzi na pia haiwi kazi ngumu kuingiza.
Uume wake ulikuwa unaonekana umesimama sana ila hauingii unakua kama hauna nguvu.
Huyu
mwanaume alinitesa kweli kihisia kwani nilikua na ham sana lakini
ndio hivyo hawezi kuingiza nakuiacha peke yake ....lazima aishikilie na
mkono na ananifuta uchi uwe mkavu ndio ajaribishe kuingiza....
Yaani
kuna mda tulikuwa tunafikia mpaka tunaamua kuacha kwani hafanikiwi
kuingiza anajishikilia kwenye kichwa anaingiza kichwa kidogo.
Nakumbuka nimeshawahi kuwa nae siku mbili lakini alifanikiwa kuingiza mara moja na hakukaa hata dakika kumi ikatoka.
Alafu sijawahi muona akipiga bao zaidi ya mara moja tu .JE, hili ni tatizo gani kwa mwanaume huyu?
Ukimuangalia
ni handsome, ananguvu za kutosha tu na uume wake unasimama vizuri na
ni mkubwa vizuri na isitoshe nilikuwa namfanyia blow job ya kutosha na
nampa romance ya kutosha kuhakikisha yuko tayari lakini wapi.
Mwenzenu
yaliyonipata ndio hayo, Ingawa yule mwanaume niliachana naye ila kila
siku nimekuwa nikifikiria je hili ni tatizo gani? Nimekaa na siri moyoni lakini kwa kweli imenishinda .
Na sio kwamba umri wake ni mkubwa ni bado kijana mdogo hajafika hata
miaka thelathini, kwa mnaojua labda nini atumie ili awe anajiweza
kimapenzi hata nijaribu kumshauri kwani nasikia hata msichana aliyenae
sasa ameshaanza kulalamika kwa watu.
Na sikupenda lile tatizo lake kwani wakati wa tendo alikua anahangaika
sana utamuonea huruma na tunaishia tu kujaribu kuingiza hatufanikiwi
kufanya.
Asanteni.
USHAURI WA TATIZO:
Hili tatizo lipo kwa kiasi kikubwa sana miongoni mwa wanaume lakini
kutokana na UANAMUME huwa hawapendi kulizungumzia sio kwa wapenzi wao
tu bali hata kwa madaktari.
MTAZAMO
HUYO MTU ANATATIZO LIITWALO PARTIAL IMPOETANCE.
HUSABABISHWA NA VITU VINGI,WOGA WA MUNGU,WOGA WA MAHALI PA KUFANYIA TENDO,
WOGA
WA MAGONJWA,WOGA KWA MSICHANA KWA MAANA YA KUOGOPA KUUMBUKA AU
KUMKAMIA SANA MSICHANA AU KWA KUTAKA KUMWOMYESHA BINTI KUWA ANAYAWEZA.
NA MSONGO WA MAWAZO KWA UJUMLA.PIA HUTOKEA KAMA MTU HAJAMFEEL SANA MTU AU ANASUTWA NA NAFSI KWA KUTAKA KUIBA NGONO.
NYONGEZA YA VISABABISHI.
1)-Maumbile ambayo wengi wanarithi.
2)- Mtu aliyezoea kupiga punyeto kwa muda mrefu
3)- Matatizo ya Kisaikolojia yaliyosababishwa na wanawake (ana historia mbaya na wanawake),
3)-Kuugua kwa muda mrefu huko nyuma (matokeo ya matumizi ya dawa mbali mbali),
4)-Kutojiamini,
5)- Wewe kutokuwa "relaxed" yaani unanyege na uko mnyevu lakini pia uko
"tense" hatoweza kuingia na jinsi anavyojitahidi kuingia anashindwa
inampunguzia kujiamini hata kuhisi kuchoka na kupoteza ugumu wa uume
wake.
6)-Stress kutokana na maisha au shughuli za kimaisha na kazi.
7)-Kutokujua afanyacho (sio mzoefu sana) na labda anajua wewe mambo yako yako juu.
8)-Umri mdogo kitu kinachoweza kusababisha yeye kutokuwa tayari kwa
tendo au kuwa kenye uhusiano wa kimapenzi na ngono......nakadhalika.
NINI KIFANYIKE?
Kutokana na umri mdogo wa mpenzi wako huyo wa zamani sidhani kama ni
busara kumshauri kutumia dawa za kuongezea nguvu zile za kisasa au za
kienyeji za kiume kabla ya kujaribu njia za kawaida ambazo hazina
madhara .
Njia hizo ni kujitahidi na kujua hali yake hiyo inasababishwa na nini
hasa? Na hilo litafanikiwa ikiwa ataondoa aibu na kuweka pembeni "ego"
yake na kwenda kumuona Daktari na kumueleza yaliyomsibu huko nyuma kama
yapo(Kisaikolojia), Kinachompata anapokuwa na wewe (labda
kutojiamini/uoga), amewahi kuugua alipokuwa mdogo, kuna matatizo ya
kiafya kiukoo kama kisukari n.k
Sasa kwa vile hana mpenzi kwa sasa na wewe inaonyesha unampenda,
unamjali na kutaka kumsaidia basi sio mbaya kama mkarudiana (sio lazima
) ukamsaidia kwa kutumia bidhaa iitwayo "cock ring"..
Inapatikana kwenye maduka ya dawa sambamba na Condom lakini "pete ya uume"
hiyo husaidia kuufanya uume kubaki mgumu kwa kutoruhusu damu iliyojaa
uumeni kushuka chini nakusababisha "kiungo" kulegea au kupoteza u-firm
wake.
Kifaa hiki huwekwa chini kabisa karibu na pumbu pale uume unaposimama na kukaza hali itakayomfanya mwanaume asimamishe kwa muda mrefu kuliko kawaida yake na haina maumivu yeyote kwako wewe wala yeye mwanaume kwani bidhaa hiyo imetengenezwa kwa mpira.
Vilevile ajitahidi kula vyakula vyene vitunguu saumu, apendelee kula vyakula vya baharini hasa pweza.
ASANTENI.
NJIA ZA KUFANYA MATITI YASILALE
Ikiwa
wewe umechelewa(ulikuwa hujui hili wakati matiti yako yanaota) basi
msaidie mdogo wako au binti yako anaekuwa hivi sasa, ili asije
kujisikia vibaya pale wanaume watakapokuwa wakiponda matiti kwa
kuyaita "malapa"....
 |
|
Kwanza
kabisa hakikisha mtindo wa kulala ni kifudifudi (kulalia tumbo), kwa
kufanya hivyo kunasaidia kwa kiasi kikuwa kufanya matiti yako pumzike,
kwamba hakutakuwa na kuning'inia kama utakuwa umelala chali(lalia
mgongo) au kiubavu.
Zoezi...1
Asimame
wima dhidi ya mlango au ukuta kisha aegeshe matiti yake mahali hapo
kwa nguvu kisha aachie (ajitoe ukutani), zoezi hili hufanya matiti
yaume sana lakini wewe kama dada mpe moyo kuwa avumilie. Afanye hivyo
mara 20 kila asubuhi.
Zoezi....2
Simama wima huku
mikono yako ikiwa imenyooshwa huku na kule kisha ipeleke mbele
nakukutanisha viganja vyako alafu irudishe nyumba kadiri uwezavyo (sio
lazima ikutane) ila utahisi maumivu fulani sehemu ya matiti (misuli
yafanya kazi hapo)....fanya hivyo mara 10 na ongeza hesabu njinsi
unavyokua.
Zoezi...3
Ukiwa
umesimama wima na mikono yako imenyooshwa huku na hule inanyue
taratibu kuelekea juu na kutanisha vidole vyako huko juu kisha rudisha
mikono ilipokuwa (imenyooka huku na kule).