HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Saturday 4 June 2016

Hii video mpya ya Abdu Kiba ‘Bayoyo’ itazame hapa,Enjoy.

Jii video mpya ya Abdu Kiba “BAYOYO” imetayarishwa na Hanscana. Bonyeza Play Kuitazama.

VIDEO: Magoli ya mechi ya Taifa Stars vs Misri June 4 2016, Full Time 0-2


 

June 4 2016 timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ilicheza mchezo wake wa tatu wa Kundi G wa kuwania kufuzu michuano ya mataifa Afrika 2017 AFCON dhidi ya timu ya taifa ya Misri uwanja wa Taifa Dar es Salaam, mchezo ulimalizika kwa Misri kuibuka na ushindi wa goli 2-0, magoli ambayo yalifungwa na Mohamed Salah dakika ya 43 na 5
ALL GOALS: Azam FC Vs Esperance ya Tunisia April 10 2016 (Full Time 2-1)

Video: Fetty Wap – Wake Up

School’s out and Fetty Wap is saluting the Class of 2016 in the video for “Wake Up.” The Remy Boy reminisces on his high school days by returning to his alma mater, Eastside High School in Paterson, New Jersey, which inspired the film Lean on Me. Before he was a world famous star, the self-described “nobody, high school dropout” was just a kid with big dreams

Ronaldinho kutokea kwenye filamu mpya ya Van Damme


Staa wa soka duniani, Ronaldinho Gaucho amekubali kucheza kwenye filamu mpya ya kikckboxer ‘Retaliation’ ya Jean-Claude Van Damme.
34BCBF5400000578-3619134-It_was_only_earlier_this_year_that_she_found_love_with_portly_Ro-m-43_1464755344478
Ronaldinho ambaye kwenye filamu hiyo ametumia jina la Ronaldo atakuwa pamoja na mastaa wengine kama Mike Tyson, Fabricio Werdum na Paige Van Zant.
Producer Rob Hickman kutoka Hollywood amesema, “As producers, much like advertisers and brands, we must look at a potential star’s total value. In addition to his charisma, Ronaldinho also brings with him 66 million social media followers from all parts of the globe. Those numbers are an element that a lot of traditional movie stars can’t offer and when we market the film, that is something that will be invaluable.”

VideoMPYA: Quick Rocka, G Nako na Jux wametuletea hii video mpya ya ‘hapo


TV zinazidi kupata ugeni wa video mpya za bongofleva ambapo time hii ni zamu ya Quick Rocka G Nako na Jux kwenye single mpya inaitwa ‘hapo’, ukishamaliza kuitazama uniachie na comment yako umeionaje na wimbo wenyewe

Friday 3 June 2016

VIDEO: Meno ya gold ya Diamond yaonekana akimuongelea Harmonize na Korede

Kupitia Twitter yake Diamond aliandika kuhusu ngoma itayowakutanisha wakali wawili ambao ni Harmonize wa Tanzania na Korede wa Nigeria, sasa AyoTV imempata kwenye Exclusive Interview na kuelezea ambapo pia muonekano wake ulionekana ukiwa na mabadiliko ya meno ya Gold, tazama hii video hapa chini

Video: Party iliyofanyika nyumbani kwa Diamond Platnumz ya Kumkaribisha Rich Mavoko



June 2 2016 Ndio siku rasmi ambayo Lebel ya WCB ilimtambulisha Rich Mavoko kama msanii wa lebel hiyo, mtu wangu baada ya utambulisho huo uongozi wa WCB uliamua kufanya party ya Kumkaribisha Rich Mavoko pamoja na mke wa Meneja wa Harmonize (Ricardo Momo) kwenye familia hiyo, party ambayo ilifanyika nyumbani kwa Diamond Platnumz ULIMISS UTAMBULISHO WA RICH MAVOKO RASMI WCB ITAZAME HII VIDEO HAPA CHINI.

Picha: Michael Jordan aungana na Neymar kutengeneza viatu vipya vya Nike




Staa wa soka wa timu ya Barcelona, Neymar na legend wa mchezo wa kikapu duniani, Michael Jordan wameungana kutengeneza viatu vipya vya soka vya ushirikiano wa Nike/Jordan.
image
Mshambuliaji huyo wa Brazil anakuwa mcheza soka wa kwanza kuhusishwa kwenye viatu vya Jordan.
Namba 23 aliyokuwa akiitumia Jordan enzi zake ni maarufu nyuma ya viatu hivyo pamoja namba 10, namba anayovaa Neymar anapoichezea timu yake ya taifa.
image
Wawili hao waliamua kufanya kazi pamoja kutengeneza kiatu kipya kutokana na kuheshimiana kwao kwa mafanikio waliyoyapata kwenye michezo yao.
image
Viatu hivyo viitwavyo Jordan V vitatoka vikiwa na jina la Neymar kwenye ulimi wake.
Neymar ameandika herufi za jina la mwanae, DL (David Lucca) na bendera ya Brazil kwenye viatu hivyo.
image
‘I’m excited that Neymar and the Jordan Brand are working together. ‘I’m a fan of his creativity, style and passion for the game of soccer. He’s a special player and I look forward to this collaboration,” alisema Jordan.
Naye Neymar aliongeza: ‘Michael Jordan set the standard for greatness. He’s an incredible competitor and a champion. I’ve always admired him, so to collaborate with him and have his icon on my boots means a great deal to me.’
Neymar, ambaye kwa sasa yupo likizo Marekani, atavivaa viatu hivyo kwenye michuano ya Olimpiki mwaka huu.
Viatu hivyo vinavyouzwa kwa $190 vimeanza kupatikana leo June 3 kupitia Nike.com.

Thursday 2 June 2016

Picha: Diamond aitambulisha rasmi label ya WCB pamoja na ‘kumsainisha’ Rich Mavoko




Diamond Platnumz Ijumaa hii ameitambulisha rasmi label yake ya ‘WCB’ pamoja na kumsaini Rich Mavoko mbele ya waandishi wa habari.
Rich Mavoko akisaini mbele ya
Rich Mavoko akisaini mbele ya Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa, Godfrey Mngereza
Aidha, Diamond alimtambulisha dada yake, Queen Darleen kuwa mmoja kati ya wasanii wapya wa label hiyo.
Shughuli hiyo ilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa, Godfrey Mngereza ambaye alizungumza na kumpongeza Diamond huku akiwataka wasanii wengine kushirikiana kwa namna hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari katika hoteli ya Regency Park jijini Dar es salaam, Diamond amesema WCB imemsani Rich Mavoko ili kuleta chachu katika muziki.
“Nia ya kuwaita hapa ni kuonyesha kwamba wasanii tunaweza kushirikiana, tunaweza kufanya kitu kikubwa, ni muda wa kuonyesha sio ulimwengu wa vita kwa wasanii, watu wachukiane,” alisema Diamond. “Tukishirikiana wasanii kwa wasanii tutaonyesha mfano bora kwa jamii na hata mafanikio yataongezeka, kwa hiyo tuna Richard hapa na tunamshukuru sana, karibu kwenye familia,” alisema Diamond.
Kwa upande wa Rich Mavoko ameshukuru kusainiwa na WCB, huku akiwaahidi mashabiki wake mambo mazuri
“Mimi nizishukuru media zote ambazo zimefika kwenye shughuli hii maalum. Mimi nafikiri leo ni siku kubwa sana kwangu, kwa WCB pamoja na kwa tasnia ya muziki kwa ujumla. Lengo letu kubwa ni kuonyesha kwamba muziki wetu umefikia kwenye biashara kubwa sana, sisi tukionyesha umoja hata serikali itaweza kutusupport. Kwa hiyo sisi wasanii wenyewe kwa wenyewe tunabidi tuonyeshe undugu, pia serikali itaona sisi tupo serious kwenye kazi, kwa hiyo lengo la kuwa na Nasib WCB ni kufanya naye kazi, na nahaidi kufanya kazi nzuri zaidi ili kufikisha muziki wetu sehemu fulani,” alisema Rich Mavoko.
Pia Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza ambaye alihudhuria shughuli hiyo, alimpongeza Diamond huku akiwataka na wasanii wengine kushirikiana ili kuleta chachu kwenye muziki.
“Ni vizuri sana tunapo waona wasanii watanzania wanawekeza katika industry ya muziki, kwa hatua hii inaondoa ile dhana kwamba wanaoweza kuwekeza kwenye muziki ni watu toka nje, kwa hiyo ni hatua kubwa sana, ni hatua ya msingi sana ambayo Diamond na team yake yote wameipiga katika kuonyesha dhahiri kwamba kila kitu kinawezekana,” alisema Mngereza
Mavoko ambaye pia amechia wimbo uitwao ‘Story’, amesaini mkataba wa miaka 10.
Pia mmoja kati ya mameneja wa WCB, Sallam alisema mkataba huo haujamfunga Rick Mavoko kuondoka WCB, kama akihitaji kuondoka itabidi anunue mkataba huo ndipo aondeke.
Diamond na Mavoko wakibadilishana mikataba
Diamond na Mavoko wakibadilishana mkataba
Diamond na Mavoko wakipongezana
Diamond na Mavoko wakipongezana
Mavoko akisaini
Mavoko akisaini
Queen wa WCB

Tazama behind the scenes ya video ya Moyo Mashine ya Ben Pol,

Ben Pol ametupeleka nyuma ya utengenezaji wa video ya hit single yake, Moyo Mashine iliyofanyika Afrika Kusini na kuongozwa na Nic. Utagundua mambo mengi sana ambayo ulikuwa huyajui kuhusu video na wimbo huu. Tazama hapo chini

Picha: Mpenzi mpya wa Nuh Mziwanda ajichora tatoo ya Nuh



Baada ya Shilole kujichora tatoo ya Nuh Mziwanda enzi alipokuwa mpenzi wake, mpenzi mpya wa muimbaji huyo wa ‘Jike Shupe’, naye kajichora tattoo ya Nuh kwenye mkono wake.
nuh-mziwanda-2
Shilole alichora tatoo lakini baadaye ilikuja kumgharimu walipo achana Nuh. Matokeo yake tatoo hiyo iliyokuwa kifuani Shishi aliibadilisha na kuwa ua, je na huyu naye itakuwaje?
Msichana huyo amejichora kwenye mkono wake shishi

Video: Rich Mavoko – Ibaki Story


 

Msanii Rich Mavoko ametambulishwa rasmi June 2 2016 atakuwa chini ya lebo ya WCB inayosimamiwa na Diamond Platnumz, Rich kaachia video yake mpya inaitwa ‘Ibaki Story’ ambayo imefanyika Johannesburg South Africa.

Rapa M 2 The P kazitaja kazi tatu maarufu zinazofanywa na vijana wakitanzania nchini South Africa

Msanii wa rapa kutoka Tanzania anaye fanya kazi zake za muziki nchini Afrika kusini amezitaja kazi tatu maarufu sana kufanywa na vijana wa kitanzania wanaokwenda Afrika Kusini kutafuta kazi.
Pia M 2 The P anasema vijana wengi kutoka Tanzania wanaoishi Afrika kusini wamekuwa wakipata mashavu ya kazu hizo kutokana na ujanja wao wa kuweza kuishi na watu tofauti na kuongea lugha zao

Facebook inatumia simu za watu kusikiliza wanachozungumza, asema Profesa



Facebook inasikiliza mazungumzo ya watu muda wote, mtalaam wa masuala ya teknolojia ameonya. App hiyo inadaiwa kutumia simu za watu kukusanya taarifa ya kile wanachokizungumza, imedaiwa.
image
Kwa upande wake Facebook inadai kuwa app yake inasikiliza kinachotokea duniani lakini kama njia tu ya kuona nini watu wanasikiiza au kuangalia kwenye tovuti hiyo.
Kitu hicho kimekuwepo kwa miaka sasa lakini onyo la hivi karibuni la Kelli Burns, profesa wa mawasiliano katika chuo kikuu cha South Florida, limetiliwa mkazo.
Profesa Burns amedai kuwa kifaa hicho kinatumia sauti inayoichukua si  kuwasaidia watumiaji, lakini kinaweza kuwa kinafanya hivyo kusikiliza mijadala na kuitunza kwaajili ya matangazo. Amesema kujaribu uwepo wa kitu hicho, alijadiliana mada kadhaa karibu na simu na kisha kugundua kuwa tovuti hiyo imeonekana kuonesha matangazo yanayohusiana na alichokizungumza.
Madai hayo yanaendana na ripoti zilizopo kuwa tovuti hiyo huonesha matangazo ya vitu ambavo watu wamevitaja kwenye mazungumzo yao. Facebook imedai kuwa husikiliza sauti na kukusanya taarifa kutoka kwa watumiaji lakini haitumii sauti hizo kuamua kile kinachoonekana kwenye tovuti.
Kwa sasa kifaa hicho kinapatikana Marekani tu.
May 31 2016 wizara ya  mambo ya mje na ushirikiano wa Afrika Mashariki iliwasilisha hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 na Wabunge wakaanza kutoa michango yao.
Mbunge wa Mchinga Hamidu Bobani alisimama kuhoji ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa jimboni kwake kuhusu kumrudisha mjusi mkubwa wa kihistoria aliyechukuliwa Tanzania na kupelekwa Ujerumani.
Suala la mabaki ya mjusi wa Tendeguru yaliyopo Ujerumani, tuna mabaki ya mjusi yamechukuliwa Tanzania nyie mnakaa hapa kusifia tu, nimeandika barua kuwaletea makatibu wakuu walichonijibu sikielewi
‘Haiwezekani mjusi huyu mkubwa anaijengea historia Ujerumani, watalii wanaenda kuangalia wanaingiza pesa, Rais Magufuli aliahidi wakati wa kampeni kuwa atalishughulikia, haiwezekani kama taifa tunakaa tu vitu vyetu vinawanufaisha watu wengine’

VIDEO: Mambo mengine manne ya Mbunge wa ‘sanamu ya Diamond’ bungeni


Baada ya May 31 2016 Wizara ya mambo ya mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki kuwasilisha hotuba yake ya makadirio ya mapato na matumizi ya kiasi cha shilingi 151,396,775,000.00 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kupitia kwa Waziri wake Augustine Mahiga.
Wabunge mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia bajeti hiyo, mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga pia alikuwa mmoja wapo ambapo yeye alikuwa na mambo yake makubwa manne aliyotaka Wizara ihakikishe imeyashughulikia ikiwemo suala la watanzania wanaofungwa nchini China.


Alikiba katangaza utaratibu atakaotumia kuanza kufollow mashabiki wake

Perfect Crispin ni mtangazaji wa Clouds FM ambaye hapa anatusogezea stori zilizochukua headlines kutoka kwenye tasnia ya Bongo Fleva, ambapo leo June 1 2016 ametusogezea hizi stori tatu ikiwemo ya utaratibu ambao Alikiba kaandaa kwa ajili ya kuanza kuwafollow followers wake.
“Nipo na utaratibu wa kuanza kuwafollow followers wangu kwa ajili tu ya kushow love na kila siku itakuwa na utaratibu wake kwa wiki labda nakuwa na mfollow mtu mmoja halafu namtoa angalau watu waone kama kuna mtu fulani nilimfollow ila lazima awe shabikiwa Alikiba”

BET wampa shavu mtoto wa Diamond, Tiffah

Nina miaka zaidi ya 10 kwenye tasnia ya habari lakini sijawahi kupata umaarufu kama alioupata mtoto wa Diamond Platnumz, Tiffah. Wanasema mtoto wa nyoka naye ni nyoka, hivyo kuwa binti wa mwanamuziki maarufu Afrika kama Diamond umaarufu si kitu kinachoepukika.
CjxfYMaUUAAvYyx
Wiki hii kituo cha runinga cha BET tawi la Afrika kimempa shavu mtoto huyo mwenye takriban miezi kumi sasa kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii.
“Our #CuteDay snap is baby Princess Tiffah, @diamondplatnumz’s bundle of cuteness. RT to share the cuteness,” wameandika BET kwenye picha ya mtoto huyo iliyowekwa Instagram na Twitter.
Mama yake, Zari ameirepost pia picha hiyo kwenye Instagram.
Diamond ametajwa tena mwaka huu kuwania tuzo za BET kwenye kipengele cha Best International Act: Africa

Videos Video: Baada ya Rayvany kuachia ‘Natafuta kiki’ Mchekeshaji Stan Bakora kaifanyia video..

Baada ya Msanii kutoka  lebel ya WCB Rayvany kuachia hitsong yake ya  ‘Natafuta Kiki‘ leo June 1 2016 mchekeshaji Stan Bakora anatualika kwenye video yake aliyoifanya kupitia hitsong ya wimbo huo ‘Natafuta kiki’, mtu wangu usisahau kuniachia comment yako hapa wakali hao wataziona hapa

Tuesday 31 May 2016

Sababu za Diamond Platnumz kutokuwa na dream ya kuwa chini ya record label yoyote


Perfect Crispin ni mtangazaji wa Clouds FM ambaye hapa anatusogezea stori zilizochukua headlines kutoka kwenye tasnia ya Bongo Fleva, ambapo leo May 31 2016 ametusogezea hizi stori tatu ikiwemo ya Diamond Platnumz kutokuwa na mpango wa kuwa chini ya lebel yoyote.


‘Dili nililopata hajawahi kupata msanii yeyote tangu muziki wa bongo fleva umeanza‘:-Diamond Platnumz
Stori zilizochukua headlines kutoka kwenye tasnia ya Bongo Fleva, ambapo leo May 31 2016 ametusogezea hizi stori tatu ikiwemo ya Diamond Platnumz kutokuwa na mpango wa kuwa chini ya lebel yoyote. ‘Dili nililopata hajawahi kupata msanii yeyote tangu muziki wa bongo fleva umeanza‘:-Diamond Platnumz ULIIKOSA HII YA VANESSA MDEE KUONGEA KUHUSU BEEF NA SHILOLE? UNAWEZAA KUANGALIA VIDEO HII HAPA CHINI

Lionel Messi na baba yake wamefikishwa tena Mahakamani leo May 31 2016

Mchezaji wa kimataifa wa Argentina anayeichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania Lionel Messi na baba yake mzazi Jorge Messi wanatuhumiwa kwa kosa la ukwepaji kodi na leo May 31 2016 inaripotiwa kesi yao kuanza kusikilizwa katika jiji la Barcelona Hispania.
Messi ambaye ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia mara tano, anajiandaa na michuano ya Copa America itakayofanyika mwaka huu USA, lakini kesi inayomkabili ya ukwepaji kodi wa Pound milioni 3.2 ambazo ni zaidi ya bilioni 10 za kitanzania imeanza kusikilizwa.
34CA3C8E00000578-0-image-a-5_1464697218179
Mwanasheria wa Messi na baba yake akizungumza na vyombo vya habari kwa niaba ya staa huyo na baba yake.
Kiasi cha kodi wanachodaiwa Messi na baba yake, walikwepa kulipa kodi hiyo kati ya mwaka 2007 na 2009 wakati mauzo ya picha za staa huyo wa FC Barcelona, ofisi ya waendesha mashtaka wamependekeza Lionel Messi na baba yake wahukumiwe miezi 22 jela.


Mchekeshaji Joti katuletea hii ya Mwanamke wa mjini alivyokutana na Cha Mkongo..+Video

Inawezekana siku yako haijawa poa sana leo, basi chukua time hii kuirejesha furaha kwa kucheka na  vituko vya mchekeshaji Joti ambaye time hii amecheza kama mwanamke aliyekutana na Cha Mkongo sasa anamsimulia rafiki  yake kile kilichotokea baada ya tukio hilo.
Itazame hii video hapa

Picha/Video: Gorilla aliyeuawa baada ya mtoto kuangukia kwenye zoo azua mjadala duniani

Walinzi wa zoo waliompiga risasi na kumuua gorilla Jumamosi baada ya mtoto wa kiume mwenye miaka minne kuteleza na kuangukia kwenye eneo lenye mawe na maporoko ya maji alilokuwa akitunzwa huko Cincinnati, Marekani wamesababisha mjadala na hasira kali duniani kutokana na uamuzi huo.

34BD01DF00000578-3615783-The_zoo_shot_the_beloved_animal_after_he_dragged_the_boy_through-a-3_1464591377084
Familia hiyo ilienda kutembea kwenye zoo hiyo Jumamosi iliyopita na ndipo mtoto wao alipoteleza na kuanguka kwenye eneo alipokuwa mnyama huyo. Mtoto huyo alichukuliwa na kupelekwa kwenye hospitali ya watoto na kuruhusiwa jioni ya siku hiyo.
Familia hiyo ilitoa shukrani kwa waangalizi wa zoo hiyo.
“We are so thankful to the Lord that our child is safe. He is home and doing just fine. We extend our heartfelt thanks for the quick action by the Cincinnati Zoo staff. We know that this was a very difficult decision for them, and that they are grieving the loss of their gorilla. We hope that you will respect our privacy at this time.”
Baadhi ya watu wanadai kuwa wazazi wa mtoto huyo wanapaswa kukamatwa kwa uzembe wao.
34C650F800000578-3616453-image-a-56_1464634975377
Ombi la mtandaoni (petition) lililopewa jina ‘Justice for Harambe’ limepata sahihi zaidi 100,000 ndani ya saa 48. “This beautiful gorilla lost his life because the boy’s parents did not keep a closer watch on the child,” inasema petition hiyo.
34C655C300000578-3616453-image-a-54_1464633222408
Na sasa mtandao wa Daily Mail umebaini wazazi wa mtoto huyo kuwa mama yake Michelle Gregg, 32 na mume wake Deonne Dickerson, 36, mwanaume ambaye inasemekana ana historia ya matukio ya kihalifu.
34C8870D00000578-0-image-a-1_1464652047487
Wazazi wa mtoto huyo
Makosa aliyowahi kutuhumiwa kufanya ni pamoja ujambazi, makosa ya kutumia silaha za moto, biashara ya madawa ya kulevya na mengine. Mkurugenzi wa Cincinnati Zoo, Thane Maynard amedai kuwa uamuzi waliochukua kumuua mnyama huyo mwenye miaka 17 aitwaye Harambe ulikuwa sahihi ili kumlinda mtoto huyo aliyekuwa hatarini. Video zinamuonesha Harambe akimvuta mtoto huyo majini. Waangalizi wa zoo hiyo walimpiga kwa gobole na kumuua. Tukio hilo limesababisha hasira mtandaoni kuhusu kuuliwa kwa Harambe na huku wengine wakiwalaumu wazazi wa mtoto huyo. “That child’s life was in danger. People who question that don’t understand you can’t take a risk with a silverback gorilla — this is a dangerous animal. Looking back, we’d make the same decision. The child is safe,” alisema Maynard.

Justin Bieber matatani kwa kudaiwa kukopi vionjo kwenye wimbo wake Sorry

Justin Bieber anashtakiwa na mwanamuziki anayedai kuwa wimbo wake Sorry umekopi moja ya nyimbo zake.
rs_634x846-160210112459-634.Justin-Bieber-FB-021016
Muimbaji huyo, White Hinterland anaamini kuwa Justin, na producer wa wimbo huo, Skrillex, walikopi vionjo kwenye wimbo wake Ring The Bell na kutumia kutengeneza hit hiyo ya mwaka jana.
Hinterland ambaye jina lake halisi ni Casey Daniel anataka alipwe fidia.
“The writers, producers, and performers of Sorry did not obtain a license for this exploitation of my work, nor did they obtain or seek my permission,” Casey aliandika kwenye Facebook.
“Like most artists that sample music, Bieber could have licensed my song for use in Sorry. But he chose not to contact me.”
Casey anadai kuwa alijaribu kuwasiliana na Justin Bieber na timu yake chini kwa chini kabla ya kuchukua hatua za kisheria.
“After the release of Sorry, my lawyers sent Bieber a letter regarding the infringement, but Bieber’s team again chose to ignore me,” aliongeza I offered Bieber’s team an opportunity to have a private dialogue about the infringement but they refused to even acknowledge my claim, despite the obviousness of the sample. Justin Bieber is the world’s biggest artist, and I’m sure that he and his team will launch a full attack against me.”
Mashabiki wa Justin wameshaanza kumtukana mwanamuziki huyo.
“Sorry you have no talent, but don’t bring others down because they have what you want but you have zero ability to achieve,” aliandika Taryn Quinn.
“You really think Justin Bieber and Skrillex would rip you off?”
Anasema Alec Burriss. “They’ve never even heard of you, don’t worry. There’s only so many pop melodies you can write, get over yourself.”
Zisikilize nyimbo hizo hapo chini.

Video: Diamond awaomba radhi mashabiki wa Dallas Texas baada ya show yake kukatishwa

Msanii wa muziki anayefanya vizuri kimataifa, Diamond Platnumz amewaomba radhi mashabiki wake wa muziki wa Dallas Texas, Marekani baada ya show yake ya Mei 28 kukatishwa kutoka na ukumbi kwa mdogo na kufanya usalama wa watu kuwa mdogo.
Diamond Texas
Muimbaji huyo amewataka maandaaji wa matamasha kuandaa show zao kwenye kumbi kubwa kwa kuwa muziki wa Watanzania umekuwa.
Kupiti facebook Diamoand alipost picha na kuandika:

Hii likuwa show yetu ya Juzi 28th May Dallas Texas… Ila ilibidi show hii isitishwe njiani kwakuwa watu walijaa sana kupelekea wengine kukosa tiket na Kubaki milangoni, na hata walio kuwa ndani kukosa nafasi na Mbanano uliopelekea vurugu na Kushindwa kuendelea na Performance…. Hakika muziki wetu umekuwa sasa ndugu zangu waandaaji nafikiri mtuongeze kumbi kubwa zaidi watu waweze kuburudika vya kutosha!

Mtoto wa kiume wa mwaka mmoja India abainika kuwa na nywele za sehemu za siri na hamu ya ngono

Mtoto wa kiume mwenye umri wa mwaka mmoja nchini India aliyebainika kuwa na nywele kwenye sehemu zake za siri na hamu ya kufanya mapenzi amegundulika kuwa na tatizo la homoni ambalo ni nadra sana.
34C56F6700000578-3616389-The_toddler_known_only_as_Akash_was_found_to_have_the_testostero-a-22_1464615966532
Mtoto huyo ambaye jina lake ni Akash, alipatikana akiwa na homoni za testosterone zenye kiwango cha mtu mzima mwenye miaka 25. Hiyo inamaanisha kuwa alikuwa na uume wenye size kama ya mtu mzima, ndevu na nywele za sehemu za siri pamoja na sauti isiyoendana na umri wake.
Madaktari sasa wanadai kuwa mtoto huyo ana tatizo liitwalo precocious puberty ambapo mtoto hubalehe kabla ya miaka saba au nane.
Wazazi wa Akash mwanzoni waligundua kuwa kuna kitu hakipo sawa kwa mtoto wao alipokuwa na miezi sita. Uume wake ulikuwa ukiwa mkubwa kuliko kawaida, wakati mwili wake ulikuwa mdogo mno ukilinganisha na watoto wa umri wake.
“Tulidhani labda alikuwa mtoto mkubwa, hivyo hatukumpeleka kwa daktari,” mama wa mtoto huyo aliliambia gazeti la Hindustan Times.
“Lakini alipofikisha mwaka mmoja, ilikuwa wazi kuwa kuna kitu hakikuwa sawa. Mama mkwe wangu, ambaye amewalea watoto kadhaa kwenye familia pia alisema ukuaji wake haukuwa wa asili. Hapo ndipo tulipompeleka kwa daktari.’
Daktari wa Akash, Vaishakhi Rustagi, ameliambia Hindustan Times kuwa tatizo hilo lina athari kwa mtoto na kwamba itafika muda atashindwa kukua na kumfanya awe na urefu wa futi 3-4 muda wote. Mtoto huyo kwa sasa anapewa matibabu.
Precocious puberty ni tatizo la nadra sana. msichana aliyewahi kuzaa akiwa na umri mdogo zaidi kuwahi kutokea ni Lina Medina, aliyezaa akiwa na umri wa miaka mitano na miezi saba huko Peru mwaka 1939, na kuwa maarufu duniani enzi hizo.
28
Wazazi wake walidhani kukua kwa tumbo lake kulitokana na uvimbe lakini baada ya tiba za mwanzo kutofanikiwa ndipo walipompeleka hospitali.Mwezi mmoja tu baadaye aliushangaza ulimwengu baada ya kujifungua mtoto wa kiume.

Picha,Wolper katambulishwa kwa wazazi wa Harmonize,sio kiki hili….



Inaonyesha kuwa makini na serious zaidi pale unapo mtambulisha mpenzi wako kwa wazazi wako kama alivyofanya bongo fleva staa Harmonize.
Wikiendi iliyopita wcb staa Harmonize alimpeleka mpenzi wake Jacqueline Wolper kwao Mtwara alikoenda kutumbuiza kwa mara ya kwanza tangu atoke na kupata umaarufu mkubwa kwenye game ya bongo fleva.
Harmonize aliandika hivi instagram “Time Ya Kumsaidia mama Harmo Kuanda Chakula Cha Usiku Mtwara Life @wolperstylish,”
Naye Wolper aliwka picha akiwa na mama mkwe wake ‘Mama Harmonize’ na kuweka ujumbe huu “I am having the best time of my life.. Nikiwa na Mama angu… Kabla hamjatoka lazima mpige story, akuchekeshe… Mjipikilishe.. Akushauri Hapa nimepata rafiki kwa kweli…I love my mama Mkwe.. Mama Raj wangu.”
Kweli sio KIKI TENA AU…….
harmo 1 harmo 2

Mix PICHA 8: Wabunge walivyoamriwa kutoka bungeni baada ya kufukuzwa kwa wanafunzi UDOM

Naibu Spika Tulia Ackson ameamuru Wabunge kutolewa nje ya bunge baada ya baadhi ya Wabunge hao kusimama kupinga kitendo cha bunge kakataa kujadili suala la Serikali kuwataka wanafunzi wa UDOM kurudi kwao ndani ya saa 24 kufuatia mgomo wa Walimu unaoendelea kwa sasa.
AW1A0974
Baadhi ya wabunge wakionekana kujadili jambo
AW1A0973
AW1A0917
Mbunge wa Chemba Juma Nkamia alivyosimama kuainzisha hoja hiyo
AW1A0956
Mbunge wa Arumeru Joshua Nassari akifafanua zaidi
AW1A0959
Baadhi ya wabunge wakitoka nje
AW1A0960
AW1A0987
AW1A0986
AW1A0984

VIDEO: Jk Comedian alivyokutana na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

May 29 2016 Rais msataafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete alialikwa na wahitimu wa Vyuo Vikuu Dar es salaam ambao ni wanachama wa chama cha Mapinduzi ‘CCM’ katika mahafali yao pia Jk Comedian alikuwepo kwenye tafrija hiyo na akapata nafasi ya kuiigiza sauti ya Jakaya Kikwete mbele yake. Tazama video hii hapa chini