HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Thursday 8 September 2016

PICHA &VIDEO: Apple wamezindua Iphone 7 na 7plus, wameainisha utofauti wake na Iphone 6

Good news kwa watumiaji wa Iphone, ambapo kampuni ya vifaa vya electronics ya Apple kupitia bidhaa zake za simu  imezindua toleo jipya la Iphone7 na 7plus ambazo zimekuwa zikisubiriwa na wapenzi wa brand hiyo ya simu huko San Fransisco, Carlifonia Marekani.apple-7
phooone
Mwenekano wa nyuma wa Iphone 7
Apple imeainisha utofauti wa Iphone 7 na 7plus kutoka kwenye Iphone6 kuanzia ubora mkubwa wa picha kwenye camera zake, fasta kwenye kuprosess data, na zimekuja katika rangi nyingi tofauti tofauti zaidi ya zile nne za mwanzo. Aidha zina uwezo wa kustahimili maji na kukaa zaidi ya dakika 30 kwenye urefu wa futi3.2, pamoja ukubwa wa memory kuanzia 32GB mpaka 256GB.rangi
Pia Imezindua Airpods ambazo ni wireless sambamba na hilo  zinatumia mfumo mpya wa flash wa (Quad-LED True Tone flash).
earphonesss
Airpods
pods
Bei zake ni kuanzia:
Euro599 kwa Iphone7 ya 32GB mpaka Euro 799 kwa 256GB
Na kwa Iphone 7plus ni kuanzia Euro 719 kwa 32GB mpaka Euro919 kwa 256GB.

Wednesday 7 September 2016

Siku chache zilizopita nilikusogezea video mpya ya single ya Dully Sykes iitwayo INDE aliyoshirikishwa msanii kutoka WCB, Harmonize sasa leo wametuletea hii behind the scenes ya video hiyo kuona jinsi ilivyokuwa katika uandaaji wa video hiyo mpya.
Video hiyo mpya imetayarishwa na Director Hascana

VIDEO: Nyumba nne walizojengewa Yamoto Band na Meneja wao……


Ni Mkurugenzi wa Yamoto Band, Said Fella ambae hivi karibuni alizimiliki headlines  baada ya kuzionesha nyumba nne mpya  mbele ya waandishi wa habari alizowajengea Yamoto Band.
Nyumba hizo nne zipo Mbande Kisewe Chalinze Dar es Salaam ambapo muda wowote zitazinduliwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.
Itazame hii video hapa uone nyumba hizo nne za Yamoto Band

Sallam, meneja wa Diamond kuja na kituo chake cha redio

Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam anatarajia kuanzisha redio yake ya mtandaoni (online radio).

13724575_856438874487280_1965556187_n
Taarifa hiyo ilitolewa na Romy Jons, anayedai atakuwa mmoja wa watangazaji wa redio hiyo itakayojulikana kama DSM FM.

Kampuni ya Apple inatarajiwa kuzindua simu zake mpya za iPhone 7 Jumatano hii huko San Francisco, California.

iphone+7s
Simu hiyo inatarajiwa kuwa na uwezo mkubwa zaidi ya ile ya iPhone 6 huku wengi wakipendelea kuona simu hizo zisiwe na tundu la kutumia headphone jack na badala yake ziwe na uwezo wa kutumia teknolojia ya Bluetooth au kutumia Lightning ambalo pia hutumiwa kuweka chaji.
Aidha simu hizo mpya za iPhone 7 zinatarajiwa kuwa na uwezo mkubwa wa kamera na huenda simu hizo zikawa na lens mbili za kamera ambazo zitamwezesha mtumiaji kupiga picha za ubora wa hali ya juu.
Uzinduzi huo unafanyika ikiwa ni siku chache zimepita baada ya mpinzani mkubwa wa kampuni hiyo ambayo ni kampuni ya Samsung kulazimika kusitisha uuzaji wa simu yake ya kisasa zaidi ya Note 7 kutokana na matatizo ya betri.
Hata hivyo wachunguzi bado wanaendelea kujadiliana kama vifaa vilivyotumika kutengenezea simu hiyo ambayo inatarajiwa kuzinduliwa kama havitaleta madhara kama ilivyokuwa kwenye Galaxy Note 7.

Snap your fingers and sing along. Desiigner’s “Tiimmy Turner” has a new remix and it features his G.O.O.D. Music boss, Kanye West.

VideoMPYA: Wanene Entertaiment wametuletea hii ‘Naipenda Dancehall’

, DJ Davizo anatualika kuitazama video yake mpya ya Naipenda Dancehall, Video ambayo imeongozwa na Director kutoka Wanene Entertaiment, pia usisahau kuniachia comment yako hapa chini na mkali huyu ataiona hapa.

Tecno wanakuletea Phantom 6, inakuja na RAM Ya 6GB na 32GB ROM.


Kuna fununu zilizosambaa kuwa tarehe 6 Septemba ndio uzinduzi rasmi wa toleo jipya la Tecno Phantom huku ikitabiriwa kuwa ya kipekee kabisa tofauti na matoleo mengine kutolewa. Uzinduzi huu umezusha uvumi mkubwa miongoni mwa wale wapenzi simu. Kama inavyotarajiiwa, Tecno Phantom 6 itaweka rekodi katika soko la simu kimataifa.
Binafsi, bahati haikuwa yangu kupata fununu kamili mpaka nilipodokezwa na baadhi ya vyanzo vya habari vya kuaminika kuwa Tecno Phantom 6 imeboreshwa na itakuwa na nafasi kubwa ya kuhifadhi kumbukumbu ikikadiriwa kuwa 6GB RAM na 32GB ROM.
Naweza nisiwe sahihi lakini pasi na shaka ninachotabiri ni kwamba Tecno Phantom itakuwa imeboreshwa zaidi kwenye uwezo wake wa kuhifadhi data yaani “Storage”. Ni adimu sana kupata simu yenye 6GB kama Tecno Phantom itakuwa na uwezo huu, itakuwa ni gumzo.
18 Processor
INAAMAANA GANI SMARTPHONE KUWA NA RAM KUBWA
Kwa uzoefu wangu, kuwa na RAM kubwa inamaana simu ina uwezo mkubwa wa kuchakata kulingana na matakwa ya mtumiaji, hii inamaanisha kwamba simu yako (Endapo utaamua kununua Phantom 6 na ninakushauri uinunue) haitokuwa inakwamakwama.  Nafahamu matoleo kadhaa ya simu zenye uwezo mkubwa wa kuchakata ambapo inaweza kuendesha hata Apps 30 tofauti kwa mpigo bila kusuasua, lakini nikupe tahadhari kwamba matumizi yako ya data yatakuwa ya kukwamakwama sana.
Wakati faida mojawapo ikiwa kuendesha App tofauti kwa mpigo, faida nyingine ni kuwa ukubwa wa RAM ya Phantom 6 inaondoa tatizo la simu kupata moto. Kwa ajili ya kawaida huu ni ujanja ambao watengenezaji wa simu wametumia teknolojia na vifaa vinavyozuia simu kupata moto kupitiliza. Hivyo, mtazamo wangu kuhusu Tecno Phantom 6 ni kwamba inaweza ikawa sio tu yenye RAM ya 6GB pia prosesa ya hali ya juu.
Tunatumaini uzinduzi huu utamaliza mzozo na uvumi unaoendelea. endapo unahitaji taarifa zaidi unaweza kutembelea mitandao ya kijamii ya Tecno kama ilivyoorodheshwa hapa chini.

Tuesday 6 September 2016

Hadi kufikia August 2016, TOP 10 ya wanasoka wanaolipwa mkwanja mrefu

Mchezo wa soka ndio mchezo maarufu zaidi, kama ambavyo ulivyo maarufu na kupendwa na watu wengi ni kawaida kuona wanasoka pia wakilipwa pesa nyingi katika vilabu vyao hata katika mikataba yao ya matangazo ya kibiashara.

Leo September 6 2016 mtu wangu wa nguvu nimekutana na list ya TOP 10 ya mastaa wa soka wanaongoza kwa kulipwa mkwanja mrefu, list kutoka mtandao wa www.alux.com hadi kufikia August 2016 hii ndio ilikuwa list ya wanasoka wanaoongoza kwa kulipwa mkwanja mrefu.

10. James Rodriguez ($21 million zaidi ya Tsh bilioni 45)

james-rodriguez-top-model_adpo15cd890c1rrua6un2uy88-768x461
James Rodriguez

9. Cesc Fabregas ($21 million bilioni zaidi ya Tsh bilioni 45)

Cesc-x-Beats-Hear-What-You-Want-1-768x575
Cesc Fabregas

8. Eden Hazard ($22 million zaidi ya Tsh bilioni 48)

hazard1-768x435
Eden Hazard

7. Luis Suarez ($23 million zaidi ya Tsh bilioni 50)

13934991186929-768x511
Luis Suarez

6. Sergio Aguero ($24 million zaidi ya Tsh bilioni 52)

pepsiAGUERO-DC-PORTRAIT_LR-768x765
Sergio Aguero

5. Wayne Rooney ($26 million zaidi ya Tsh bilioni 56)

wayne_rooney_fc247_1_18948-768x480
Wayne Rooney

4. Gareth Bale ($34 million zaidi ya Tsh bilioni 74)

Gareth-Bale-on-holiday-in-Marbella-768x534
Gareth Bale

3. Neymar Jr. ($36 million zaidi ya Tsh bilioni 78)

Neymar-Jr-8450_klein-768x512
Neymar Jr.

2. Lionel Messi ($77 million zaidi ya Tsh bilioni 168)

tumblr_mcauq5tifs1r38yfko1_1280-768x489
Lionel Messi

1. Cristiano Ronaldo ($82 million zaidi ya Tsh bilioni 179)

wx-768x497 (1)
Cristiano Ronaldo

Kionjo cha All The Way Up Remix ya Diamond Platnumz.

Bongo Fleva super staa Diamond Platnumz ametuonjesha kidogo ujio wa Remix yake ya wimbo wa Fat Joe na Remy MaAll The Way Up‘ Ft French Montana.
Kwenye instagram yake Diamond kaandika huu ujumbe pamoja na hichi kionjo “ You know i Love being crazy Sometimes ???????????? #FoolingAround #AllTheWayUp #JINI #SIMBA #VAMPIRE Mendez tell those Mother*** ka!

Diamond Platnumz ana collabo inakuja na rapa mkali kutoka Marekani….



Staa wa Bongo Fleva ambaye kwa ssa yupo nchini Marekani  Diamond Platnumz akifanya video ya wimbo wake na Neyo amethibitisha kuwa anakuja na rekodi mpya na Rapa Yo Gotti.

Kupitia Instagra yake leo September 5, 2016 Diamond Platnumz ameandika maneno hayaOne of the Realist G i ever met…. can’t wait for our Record….Let’s go get em fam!???? @Yogottikom
diamond na yo gutti 2

Baada ya miaka 56 na filamu 200, Jackie Chan atapokea tuzo ya Oscar mwaka huu.


Mwigizaji na mtayarishaji wa filamu kutika China Jackie Chan ametajwa kupokea tuzo yake ya Oscar mnamo November mwaka huu.
Wajumbe wa bodi ya Academy of Motion Picture Arts na Science wamepiga kura hivi karibuni na kuchagua watu wakupokea tuzo ya heshima ya Oscar ambao ni Jackie Chan, Frederick Wiseman, Lynn Stalmaster na Editor wa filamu Anne V. Coates.
Jackie Chan alifanya filamu yake ya kwanza akiwa na miaka 8,na atapewa tuzo hii kutokana na uwezo na muda mrefu wa kazi bora kama mwigizaji na mtayarishaji aliyefanya vizuri kimataifa.
Ameigiza na kutengeneza zaidi ya filamu 30 akiwa Hong Kong, Hii ni post ya Jackie Facebook yake nakusema ni “Miaka 56 na filamu 200 zimepita mpaka leo na ndio muda wake kupokea tuzo hii ya heshima ya Oscar“.
jchan

Audio: Mashabiki wadata na verse ya All The Way Up ya Diamond

Diamond Platnumz amejiongezea aka zingine mpya, Jini na Vampire. Jumatatu hii aliachia kipande cha verse kwenye hit single ya Remy Ma na Fat Joe ‘All The Way Up’ kilichoyakuna masikio ya mashabiki wake. Sikiliza hapo chini.

Kujamiiana na roboti kutasababisha kupungua kwa tendo hilo baina ya binadamu kufikia mwaka 2050!

Kushiriki ngono na mashine au roboti kunaweza kufanya binadamu wapunguze kufanya tendo hilo wao kwa wao ifikapo mwaka 2050, wanasayansi wameonya.

259C61D800000578-3235704-image-m-3_1442339604820
Mtaalam mmoja wa roboti amedai kuwa mapenzi na roboti yanaweza kuwa na uraibu na siku za mbele zaidi kupoteza kabisa ushiriki wa tendo hilo baina ya binadamu kwa binadamu.
Kama teknolojia zingine ambazo zimechukua kazi za binadamu, roboti wanaweza kupita uwezo wa wanaume, na kuwa wapenzi bora.
Akizungumza na Daily Star, Joel Snell, mtaalam wa roboti kutoka chuo cha Kirkwood cha Iowa, alisema: ‘ Mapenzi na roboti yanaweza kutengeneza uraibu. Roboti wa ngono watakuwa wakiwepo daima na hawawezi kusema hapana.’
Pamoja na kupatikana muda wote kwaajili ya tendo hilo, roboti wanaweza kuwa wajuzi zaidi katika mapenzi kuliko binadamu.
Snell aliongeza: Kwa sababu watakuwa wametengeneza utaratibu mahsusi, roboti wa ngono watakidhi kila hitaji la mtumiaji.’