HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Sunday 19 June 2016

Simba watatu wamehukumiwa kifungo cha maisha


Kwa kawaida wanyama wakali kama Simba, Chui, na wengine huwekwa chini ya usimamizi mkali endapo kukiwa na hatari ya kudhuru binadamu ama wanyama wanaowazunguka. Ila taarifa za kuwahukumu simba watatu kifungo cha maisha baada ya kugundulika wamemla mtoto wa miaka 14 huko India kimeshangaza wengi
Kwa kawaida tumezoea kuona Simba akiuliwa kama ikitokea kamshambulia binadamu lakini sio kufungwa, ila India wamefikia maamuzi tofauti kidogo ya kuwafungia kifungo cha maisha Simba watatu  kutokana na wananchi wa eneo hilo kulalamika kutokea kwa matukio hayo.
simba
Simba hao watatu, wawili wakiwa wakike na dume mmoja, walimshambulia mtoto aliyekuwa amelala nje ya nyumba kwenye bustani katika hifadhi ya taifa ya Gir Gujarat India. Mtoto huyo atakuwa mtu wa tatu kuliwa na Simba tangu April 2016 hali ambayo ilisababisha wananchi wa eneo hilo kuiomba serikali ichukue hatua ili kutokomeza matukio ya aina hiyo.

No comments:

Post a Comment