HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Wednesday 20 April 2016

Magodoro haya yanaweza kugundua iwapo mpenzi wako anachepuka

Watengenezaji wa magodoro wameendelea kuumiza vichwa zaidi kuingiza sokoni magodoro yanayotumia teknolojia ya hali ya juu
Mid-adult couple sleeping --- Image by © Tim Pannell/Corbis


Watengenezaji wa Hispania wametengeneza magodoro yanayoweza kugundua iwapo mpenzi wako anachepuka. Yakiuzwa kwa £1,200, magodoro hayo yanamwezesha mtu aliye mbali na nyumbani kuangalia simu yake na kuangalia kama yanatumika na watu wangapi wamelalia.
Magodoro hayo yanatumia sensa maalum kugundua matumizi yanayotia wasiwasi na kumjulisha mmiliki kupitia app.
Watengenezaji wanadai kuwa ni ngumu kugundua kwa macho kuwa magodoro hayo yamefungwa kitu kwasababu taknolojia hiyo imefungwa kwenye springi zake.
Msemaji wa kampuni ya Durmet, watengenezaji wa magodoro hayo, Jose Antonio Muinos alidai kuwa waliamua kuja na wazo hilo kwasababu takwimu za usaliti kwenye ndoa na uhusiano zinaonesha kuwa Wahispania ni watu wasio waaminifu zaidi Ulaya.
“It is a concept that will bring peace of mind to men and women, not just during the night but also during the day while they are out at work and the bed should really be being used. On the outside it is just a normal looking and very comfortable mattress, but inside hides some cutting-edge technology,” alisema.
‘We think the mattress will do well internationally because it is the only one in the world that uses this technology and is designed specifically for the objective of catching cheating partners.”
Kwa mujibu wa mtandao wa Ashley Madison, mji wa Madrid unaongoza kwa kuwa na watu wanaosaliti zaidi ndoa zao.

No comments:

Post a Comment