Mabasi hayo yameanza safari zake kwa barabara mbili kubwa, kuanzia Morocco mpaka Kivukoni na kutoka Mbezi Mwisho mpaka Kivukoni. Wananchi wengi wameonekana kufurahishwa na mabasi hayo ambayo yameonekana kurahisisha usafiri kwa kutoka muda mwingi vituoni lakini wengi wameonekana bado wakiendelea kulalamikia nauli kuwa kubwa pindi watakapoanza kulipia huduma hiyo itakuwa ni shida kwao.
Aidha mabasi hayo yameonekana kujaza muda wote wa safari huku abiria wengi wameonekana wakizunguka na mabasi hayo pasipo kushuka na kuwaacha wale wanaosafiri kweli kupata shida kwenye vituo hivyo.
Hata hivyo mabasi hayo yatakuwa na mifumo miwili ya ulipiaji wa nauli, mfumo wa kwanza ukiwa ni kulipia kwa tiketi kununua kwenye vituo vya kupandia mabasi hayo na mwingine ukiwa ni wa kulipia kwa kutumia kadi.
“Mfumo wa kadi ndiyo mfumo sahihi wa mabasi haya ila huu wa tiketi tumeuweka kwa dharura ili kuwasaidia wananchi lakini baada ya muda utaondolewa. Kuanzia kesho kadi zitaanza kuuzwa kwa shilingi 4500, lakini ndani yake kutakuwa na bonasi ya shilingi elfu mbili,” alisema mmoja wa viongozi wa kwenye vituo hivyo.
Aliongeza kuwa, “hiyo kadi ukinunua unatakiwa uanze kuiwekea hela na ukifika kwenye kituo unaingiza kadi kwenye mashine itakuruhusu uingie.”
Nauli za mabasi hayo itakuwa kama ifuatavyo; Mbezi Mwisho mpaka Morocco itakuwa ni shilingi 800, Mbezi Mwisho mpaka Kariakoo ni shilingi 800, Morocco mpaka Kivukoni ni shilingi 650, Kariakoo mpaka Morocco ni shilingi 650, Mbezi Mwisho mpaka Kivukoni ni shilingi 800 na nauli ya wanafunzi ni shilingi 200.
Tazama picha zaidi hapo chini.
No comments:
Post a Comment