HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Tuesday 5 July 2016

Kifaa cha NASA chawasili kwenye sayari ya Jupiter baada ya kusafiri kwa miaka mitano!


Baada ya safari ya miaka mitano kutoka kwenye sayari ya dunia, kifaa kinachotumia nishati ya jua, Juno kimewasili kwenye sayari ya Jupiter Jumatatu hii.
Jupiter_diagram.svg
Kwa sasa kifaa hicho kinazunguka kwenye njia kubwa (orbit) ya sayari hiyo.
Kifaa hicho kitaizunguka njia hiyo mara moja kila baada ya siku 53 hadi October 14, itakapohamia kwenye njia nyingine inayochukua siku 14. Na baada ya miezi 20 ya kijifunza kila kila kitu inachoweza ndani ya sayari hiyo na hali yake, kifaa hicho kitateketea kwenye mazingira magumu zaidi yaliyopo kwenye sayari hiyo na kukamilisha mradi huo uliogharimu dola bilioni 1.
Haya ni mambo kadhaa muhimu kuhusu sayari ya Jupiter
1. Ni sayari ya 5 kwa umbali kutoka jua letu (star).
2.Ni sayari kubwa kuliko zote ktk mfumo wa jua letu.
3.Ina miezi (moons) mingi 67 kuliko sayari zote ktk mfumo wa jua letu.
4. Ni ya 4 kwa kuwa na uangavu (brightest) wa kuweza kuonekana na binadamu bila kutumia chombo cha kuonea.
5. Mwezi wa Jupiter uitwao Ganymede ni mwezi (moon) mkubwa kuliko yote ktk mfumo wa jua letu.
6.Kati ya miezi 4 (moon) mikubwa ya Jupiter, Io,Calisto,Europa na Ganymede ni ktk mwezi Europa ndiko kunakoonekana kuwa na maisha kwa mwanadamu kwani kuna maji ya kutosha na pia viumbe hai vya kwenye maji vimegundulika kuwepo kama samaki.
7. Jupiter kwa ukubwa wake ilitosha kuwa jua (star) lakini tendo la kuwa linalizunguuka jua letu ndio limefanya likose sifa ya kuitwa jua(star)
8. Ukiwa Jupiter uzito wako ni mara 2 na nusu ya duniani,hii inamaanisha kuwa, kwa mfano kuku na kanga wetu hawawezi kuruka wakiwa Jupiter.
9. Siku (day) ndani ya Jjupiter ni fupi mno ndani ya saa 9 siku imekwi

No comments:

Post a Comment