HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Friday 22 July 2016

PICHA 6: Magari yanayotumia umeme yaanza kutumika Afrika Mashariki

Hii imeripotiwa na BBC swahili kuwa magari yanayotumia nguvu za umeme yameanza kuuzwa Afrika Mashariki kwenye  nchi ya Kenya kwa mara ya kwanza. Magari hayo hayatumii mafuta hata kidogo hii ikiwa na maana kwamba hayatoi moshi au gesi zinazochangia ongezeko la joto duniani kwa hivyo yanafaa mazingira.
Msimamizi wa kampuni Knights Energy inayohamasisha watu watumie magari ya aina hiyo, Francis Romano amesema…..>>>”Watu wengi wamekuwa wakiduwazwa na gari hili mitaani hapa jijini Nairobi na wengi wamependezwa nalo’
Bei ya gari hilo aina ya Nissan Leaf ni dola za kimarekani 10,000 ambazo ni kama Tsh milioni 21.88
160722101436_electric_car_kenya_1_640x360_bbc
Katika taarifa hii ya BBC swahili imeainisha baadhi ya faida za matumizi ya gari hilo kuwa ni pamoja na mwenye gari kutoathiriwa na kupanda na kushuka kwa bei ya mafuta pia linaendeshwa kwa njia karibu sawa na gari la kawaida.
Aidha imeelezwa kuwa gari hilo lina uwezo wa kusafiri umbali wa takriban kilomita 90 hadi 135 kabla ya betri zake kuisha chaji, kasi yake ya juu zaidi ikiwa kilomita 180 kwa saa.
160722101622_electric_car_kenya_2_640x360_bbc
Kuna baadhi pia ya changamoto ambazo mtu anaweza kukutana nazo kutumia gari hilo ambazo ni pamoja na ukosefu wa vituo vya kuchaji gari hilo na pale ambapo mtu amekwama akiwa katika maeneo ya mashambani ambapo hamna nguvu za umeme au pia vituo vya kuweka chaji.
160722102314_electric_car_kenya__3_640x360_bbc
Gari hilo lina chaji tatu, ya kwanza ina uwezo wa kuweka chaji kikamilifu kwa muda wa saa nane, ya pili ina uwezo wa kuweka chaji kwa takriban saa nne, huku ya tatu ikiwa na uwezo wa kuweka chaji kwa kati ya takriban dakika 15 na saa mbili.
160722102514_electric_car_kenya__5_640x360_bbc 160722102727_electric_car_kenya_7_640x360_bbc

No comments:

Post a Comment