HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Wednesday 13 July 2016

VIDEO: Polisi wana mpango huu kwa wale wenye vyeti feki maofisini

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam linawashikilia watuhumiwa watatu wakazi wa buguruni kwa kosa la kukutwa na nyaraka bandia za serikali kama vyeti vya kidato cha nne, stika za SUMATRA, vyeti vya vyuo vya uuguzi, vyeti vya kuzaliwa, leseni bandia za biashara, nyaraka za bima pia walikutwa na mihuri mbalimbali ya ofisi za serikali na binafsi.
Watuhumiwa wote bado wapo rumande na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani, baada ya mahojiano na polisi watuhumiw hao wamekiri kuuza vyeti watu wengi ambao wako kwenye ajira.
Akizungumza na waandishi wa habari kamishna  wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam, Simon Sirro amesema……….>>>’Wanataja na wanaendelea kutaja watu ambao wamewauzia vyeti na wameshapata ajira serikalini, kama ulinunua hiki cheti, nataka niseme ni balaa kwako kwa sababu watatutajia kila mmoja mmoja na tutakufuata huko ulipo’.
>>>’Hatuishi hizi nyaraka tulizozipata tutakwenda mbali zaidi kwa kuwanyofoa mmoja mmoja aliyejipatia kazi kwa kutumia hivi vyeti bandia

No comments:

Post a Comment