HUBATI.COM








THANK YOU FOR YOUR VISIT               

Translate

Search This Blog

Monday 4 July 2016

‘Mabasi ya haraka kuanza kutumia gesi’


Moja ya stori iliyoripotiwa ni hii kwenye gazeti la Habari Leo yenye kichwa cha habari ‘Mabasi ya haraka kuanza kutumia gesi’
Gazeti la Habari Leo limeripoti kuwa` msimamizi wa usambazaji gesi katika shirika la maendeleo ya petrol  Tanzania (TPDC), Ismail Naleja, amesema awamu ya pili ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es salaam yatatumia nishati ya gesi asilia badala ya mafuta jambo litakalosaidia kupunguza gharama.
Kupitia gazeti hilo Naleja amesema matumizi ya nishati hiyo yataanza katika awamu ya pili ambapo mabasi mapya 200 ya mradi huo yanatarajiwa kuingizwa nchini.
Akizungumza katika maonesho ya 40 ya biashara ya kimataifa ya Dar es salaam yanayoendelea kwenye viwanja vya mwalimu Nyerere, kuhusu usambazwaji wa gesi katika magari, Naleja alisema hatua hiyo itaongezeka idadi ya magari yanayotumia gesi nchini ambapo hivi sasa kuna mabasi 60 yanayotumia gesi na  kuwashauri wenye magari kutumia mfumo huo ili kupunguza gharama za uendeshaji.
>>>’‘Uendeshaji wa gesi utakua nafuu jambo linaloweza  kufanya hata nauli zake kupungua kwani kilo moja ya gesi itatumika katika umbali unaotumiwa na mafuta ya dizeli lita moja na nusu”

No comments:

Post a Comment