Wednesday, 21 September 2016
Tuesday, 20 September 2016
VIDEO: Ndege mpya ya Air Tanzania ilivyowasili Dar leo
Hatimaye mwali amewasili. Ni ndege ya kwanza ya ATCL, Bombadier Q400 NextGen.
Bombadier Q400 NextGen baada ya kuwasilia JNIA, Dar Jumanne hii
Ndege hiyo imetokea Canada ilikotengenezwa na kupokelewa kwa shangwe huku mapokezi hayo yakiongozwa na katibu mkuu wa uchukuzi, Dkt Leonard Chamriho.
Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 76.
Ndege ya pili itawasili baada ya wiki moja na Rais John Magufuli ataongoza mapokezi rasmi ya ndege hizo.
Ndege
mpya ya kwanza iliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kutumiwa na
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imetua katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam ikitokea nchini Canada
ilikotengenezwa.
Ndege hiyo
aina ya Bombadier Q400 NextGen imetua majira ya saa 6:15 Mchana na
kisha kupatiwa heshima maalum ambayo hutolewa kwa ndege yoyote mpya
inayotua katika nchi yake (Water Salute).
Baada ya
kupokewa ndege imeegeshwa katika eneo la ndege za jeshi (Airwing
Ukonga). Akizungumza baada ya kuwasili kwa ndege hiyo Katibu Mkuu
Uchukuzi Dkt. Leonard Chamriho amesema ndege ya pili inatarajiwa
kuwasili baada ya wiki moja na kwamba baada ya kuwasili ndege ya pili
ndipo yatafanyika mapokezi rasmi, yatakayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa tarehe itakayotangazwa
baadaye.
Sunday, 18 September 2016
VIDEO: TOP 10 ya nyumba za gharama zinazomilikiwa na mastaa wa Basketball
Rekodi za
mastaa wa michezo kumiliki vitu vya thamani kubwa sana yakiwemo magari
expensive, biashara za mavazi na hasa viatu na nguo zimekua zikiwekwa
kila wakati. Wapo mastaa wapya na wakongwe kama Michael Jordan
ni mmoja kati ya mastaa waliofanikiwa kuingia kwenye headlines za kuwa
na mkwanja mrefu baada ya kuendelea kushikilia deal yake na kampuni ya Nike ambao ni watengenezaji wa viatu vya Air Jordan au J 23.
Leo nakuletea list ya nyumba kumi kali sana za mastaa wa mpira wa kikapu duniani.
VideoMPYA: Diamond Platnumz na Rayvanny wanatualika kuitazama hii ‘Salome’
Wakali kutokea kiwanda cha Bongofleva Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz pamoja na Raymond a.k.a Rayvanny wakitokea katika Laber ya WCB leo September 18 2016 wanayofuraha kushare na sisi mdundo wao mpya unaoitwa ‘Salome‘
Tayari nimekusogezea hapa chini video yao, ukimaliza kuitazama niachie comment yako kuniambia wametisha kwa asilimia ngapi.
Kurekodi na Trey Songz ni mwanzo wa kutimiza ndoto yangu ya kushinda Grammy – Vanessa Mdee
Na sasa anaamini kuwa, mwanzo wa kukaribia kuiishi ndoto hiyo umewadia. Vee Money, ni mmoja wa wasanii wa Afrika, waliochaguliwa kurekodi wimbo na mshindi wa Grammy na nyota wa RnB nchini Marekani, Trey Songz. Shukrani kwa kipindi cha Coke Studio Africa (International Week) msimu wa 4, kinachomdondosha staa huyo.
Akiwa pia anawania tuzo ya Loeries za Afrika Kusini kwa kazi yake ya video bora, Niroge, Vanessa anaungana na Rema Namakula (Uganda), Yemi Alade (Nigeria), Neyma (Mozambique), Serge Beynaud (French West Africa), Lij Michael (Ethiopia), Stonebwoy (Ghana), Nyashinski (Kenya) na Emtee (South Africa) kurekodi wimbo na Trey Songz.
“Katika harakati zangu za kutafuta ushindi wa Grammy katika career yangu ya muziki, inanipa nguvu kufanya kazi kwa ukaribu na Trey Songz, ambaye alishawahi kushinda tuzo hiyo,” amesema Vanessa.
Msimu mpya wa Coke Studio utaanza mwezi ujao.
Diamond kumsaini msanii wa nje ya Tanzania, WCB
Diamond Platnumz amethibitisha kuwa kwa yupo kwenye mipango ya kuongeza nguvu kwenye lebo yake ya WCB kwa kumsaini msanii wa nje ya Tanzania
.
Hitmaker huyo wa Kidogo amesema hayo wakati akijibu swali la shabiki kwenye mtandao wa Twitter, lililokuwa linauliza “WCB hamjafikiria kusaini msanii nje ya Tanzania au mtafanya?”
Diamond alijibu swali hilo kwa kuandika, “Soon.”
Aidha muimbaji huyo amesema kuwa kolabo za wasanii wake wa WCB ambazo wamefanya na wasanii wa nje zipo tayari.
Video: Ado Tembo ft Peter Msechu – Okoa Mtoto
Tukitaka kufanya Tanzania na Afrika kuwa mahali salama
kuishi ni lazima tuanze na mtoto, nikiwa na maana tukimpenda
mtoto,tukimlinda,tukimjali na kumthamini mtoto bila shaka tutakuwa
tumefanya Africa kuwa mahala rafiki pa kuishi kwani mtoto ni Rais wa
kesho,Waziri wa kesho,Mbunge wa kesho,Dakatari wa kesho,Mwalimu wa
kesho,Ni mwanamuziki wa kesho n.k Inaanza na mimi,Inaanza na
wewe,Inaanza na yule.
Saturday, 17 September 2016
Video: P Square wameileta hii mpya inaitwa ‘Bank alert’
Behind the scenes: Video ya RayVanny ‘Natafuta kiki’
Video hiyo mpya ilitayarishwa na KWETU STUDIO
Video: Alice kella – Siri Si Siri
Msanii mwenye sauti ya kipekee katika mziki wa bongo fleva Alice kella ameachia video mpya ya wimbo “Siri Si Siri”, Video imeongozwa na Jukya kutoka Goba Studios.
Subscribe to:
Posts (Atom)